• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Dkt. Ndugulile aagiza madaktari kuchunguza ukatili kwa watoto wachanga

Posted on: June 13th, 2018

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile ameagiza wataalamu wa Afya wanapofanya uchunguzi kwa watoto waaangalie pia kama wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia hasa  ukeketaji.

Amesema hayo wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika iliyofanyika jana jijini hapa na kuongeza kuwa baada ya Ngariba kuzuiwa kufanya ukeketaji kwa vijana wa kike sasa wamebadilisha mbinu zao na kuanza kukeketa vichanga.

Amesema matukio ya ukatili wa jinsia ni mengi kuliko matukio ya ujambazi hapa nchini ndio maana Serikali  imeanzisha madawati 500 ya Jinsia kwa Jeshi la polisi kote nchini pamoja na kuanzisha namba mpya ya simu Na. 116 ambapo mtu yoyote ambaye amefanyiwa ukatili wa kijinsia anaweza kuitumia kupata msaada.

Ameongeza kuwa Serikali pia imeanzisha madawati ya kamati ya ulinzi na usalama kwa wanawake na watoto katika ngazi ya Mkoa hadi Wilaya kwa lengo la kuhakikisha haki zote za Msingi kwa watoto zinalindwa na kutekelezeka ili watoto watanzania waweze kushiriki kikamilifu katika Tanzania ya viwanda.

Pia Naibu Waziri huyo ametumia sehemu ya maadhimisho haya kuzindua kamati ya ulinzi na usalama kwa wanawake na watoto mkoani Arusha na kuwakabidhi Mwongozo uliondaliwa na Wizara  kama nyenzo ya kufanyia kazi kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Wakati huo huo Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Bi. Sihaba Nkinga katika hotuba yake kumkaribisha Mgeni rasmi amesema maadhimisho ya mtoto wa Afrika yanatoa nafasi kwetu sisi watanzania kutafakari na kujitathimini ni namna gani tunatekeleza kwa vitendo haki za Msingi za watoto.

Bi. Sihaba amesema kuwa Maadhimisho haya kimsingi yanaadhimishwa Kitaifa kila baada ya miaka mitano lakini pia huadhimishwa kila mwaka katika ngazi ya Mkoa na Wizara kwa kuzingatia agenda iliyopo hivyo Arusha inaongoza kwa mikoa mitano yenye ukatili mkubwa kwenye eneo la ukeketaji.

Amezitaja haki za watoto kuwa ni haki ya kusikilizwa, kuendelezwa, kuishi, kulindwa na kutobaguliwa lakini pia amesema kuna ukatili wa aina nyingi  akiutaja Mkoa wa Arusha kuongoza kwa vitendo vya ukeketaji.

Maadhimisho haya yanafanyika  kufuatia mauaji ya watoto zaidi ya 2,000 yaliyofanyika katika kitongaji cha SOWETO Nchini Afrika ya Kusini mwaka 1976 yaliyosababishwa na Polisi wa Serikali ya Makaburu ya wakati huo walio kuwa wanaandamana kupinga mfumo wa utoaji elimu wa kibaguzi uliokuwa unawakandamiza watoto wa kiafrika ambapo hufanyika  Tarehe 16 Juni kila mwaka lakini kwa mwaka huu yamefanyika Tarehe 13 Juni kutokana na ratiba ya serikali kuingiliana na sikuu ya Eid El Fitr.


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa