• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

IGP Sirro awataka Watendaji wa Kata,Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji kulinda na kudumisha amani

Posted on: July 2nd, 2021

Na Mwandishi wetu

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) ,Simon Sirro amewaagiza wenyeviti wa serikali za mitaa,watendaji kata na vijiji, kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kulinda amani na kutanguliza Uzalendo wa nchi ikiwa ni pamoja na kuwabaini wageni wanaoingia katika maeneo yao, ili kufichua wahalifu na magaidi kabla ya kufanya vitendo vya umwagaji damu na uporaji. 

Kamanda Sirro ameagiza kupelekwa Askari Kata ili kuweza kukabiliana na kata zenye uhalifu na ukiukwaji wa haki za Binadamu.

Akizungumza mapema leo Jijini Arusha na watendaji kata,wenyeviti wa serikali za mitaa,viongozi wa dini na polisi Jamii, IGP Sirro alisisitiza lazima wenyeviti hao wahakikishe amani na utulivu unakuwepo katika jamii zao na kujiepusha kufumbia macho matukio ya kiuhalifu na wahalifu.

"Arusha  imepakana  na nchi jirani hivyo kuingia kwa wageni wasio na nia njema na nchi yetu ni rahisi wakitokea nchi  mbalimbali kama Somalia au Msumbiji, lazima kila mmoja awe makini na wageni hao tuepuke matukio ya  miaka iliyopita ya mabomu katika maeneo mbalimbali,"alisema.

Aidha aliwataka viongozi hao kutanguliza maslahi ya Taifa na wananchi badala ya maslahi yao kwakua mstari wa mbele kufichua wahalifu na uhalifu unaofanyika katika maeneo yao.

Alisema upo uwezekano wa baadhi ya wahalifu kirudi nchini na kufanya matendo ya kigaidi,hivyo ni Vyema  kila mmoja akajipanga.

Alisema hali ya usalama kwa sasa nchini ipo shwari japo siku za karibuni kulianza kibuka matukio ya uhalifu kutokana na majambazi wengine kukata rufaa na kuachiwa huru na kuendeleza vitendo vya uhalifu 

Pia aliagiza mikutano ya kila mwezi  Kati ya Mkuu wa Polisi Wilaya(OCD) na viongozi wa ngazi mbalimbali za chini kwaajili ya kupeana taarifa za matukio mbalimbali na kuzitatua, kwani  uhalifu unaanzia majumbani,mitaani na maeneo mengine.

"Tunahimiza ushirikiano na wananchi juu ya ulinzi shirikishi kwani bado polisi ni wachache ukilinganisha na idadi ya watanzania waliopo, hivyo ushirikiano ni muhimu katika kufichua na kukomesha matukio ya kiuhalifu,"alisema.

Pia IGP Sirro aliwaonya wanaojiingiza katika matukio ya uhalifu na ugaidi kuacha mara moja, kwani hawatasalimika pale watakapokamatwa na Polisi na hakuna wa kumlaumu pale watakaposhughulikiwa.

Akizungumza kuhusu madawa ya kulevya alisema Arusha ni Mkoa wa pili au tatu, kwa uuzaji wa madawa ya kulevya hivyo ni aibu kwa viongozi waliopo sababu lazima wanawafahamu na kuwafumbia macho.

Alisema ni lazima hatua zichukuliwe ili kudhibiti matukio hayo  na  kusisitiza uimarishaji wa  doria  katika maeneo husika, ili kudhibiti suala hilo la madawa ya kulevya hasa katika Kata ya Ungalimited.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Arusha,Sophia Mjema alisisitiza umuhimu wa ulinzi na usalama ngazi za chini  ili kuleta amani na utulivu  katika kila kata na serikali za mitaa.

Wakati huo huo,Mbunge wa Arusha Mjini,Mrisho Gambo alisema Arusha ni Jiji la Utalii lakini huwezi kufanya utalii bila kuwa na amani.

Mh .Gambo aliahidi kutoa Sh. milioni 5 kwa ajili ya kituo cha Polisi Olasiti ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha Dk.John Pima alisema kuwa Uongozi wa Halmashauri  utahakikisha Ujenzi huo unakamilika  na kwa kuanzia watangia Tshs million 5 na kwamba kujengwa kwa kituo cha polisi kitasaidia kudhibiti Uhalifu .


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa