• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Maazimio kabambe ya Baraza la Madiwani (robo ya tatu - mwaka fedha 2018/2019) halmashauri ya jiji la Arusha

Posted on: May 9th, 2019

Baraza la madiwani la Halmashauri ya jiji la Arusha mapema hapo jana limefanikiwa kuketi kikao cha robo ya tatu kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya jiji la Arusha.

Wakati akifungua kikao hicho  Mstahiki Meya wa jiji la Arusha ambaye ndiye mwenyekiti wa baraza la madiwani,  Mhe. Kalist Lazaro Bukhay  amewapongeza watumishi kufuatia jiji la arusha kupata hati safi kwa miaka minne (4) mfulululizo kufuatia ripoti ya Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG)  iliyotolewa hivi karibuni.

Katika  ufunguzi wa kikao hicho  Mhe. Kalist Lazaro alisema kuwa hapingani na zoezi la utoaji wa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo (machinga) katika jiji la Arusha isipokuwa zoezi hilo limeathiri ukusanyaji wa mapato kwani baadhi ya watumishi wamekuwa wakigawa vitambulisho hivyo kwa wafanyabiashara walio na mikataba ya kisheria na Halmashauri.

Akiongeza katika hilo ametolea mfano wa makusanyo yalivyokuwa kabla na baada ya zoezi la vitambulisho kuanza katika soko la NMC,  alisema kuwa soko hilo lina vizimba 2640 na mapato yalikuwa ni shilingi milioni 21 kwa mwezi lakini hadi kufikia juzi ni wafanyabiashara wenye vizimba 40 tu ndio hawana vitambulisho hivyo kupelekea mapato kushuka hadi shilingi 10,000/= kwa siku.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa jiji la Arusha Dkt. Suleiman Madeni amekiri changamoto hiyo kwani kwa nyakati tofauti amekuwa akipokea simu kutoka kwa wakuu wa masoko wakilalamikia baadhi ya watumishi kugawa vitambulisho ndani ya masoko.

“Nimesikitishwa sana na kitendo cha baadhi watumishi wa Jiji hili kugawa vitambulisho kwa wafanyabiashara wasiostahili kwani kufanya hivyo ni kuhujumu mapato ya Halmashauri  na pia  ni kuenda kinyume na maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Jemedari Dkt. John Pombe Magufuli” alisema Dkt. Madeni

Kufuatia ajenda hiyo ya dharura iliyoanzishwa wakati wa ufunguzi wa kikao hicho Mstahiki meya wa jiji la Arusha Mhe. Kalist Lazaro Bukhay  amewataka wataalam wa Halmashauri kuandaa taarifa ya kitaalamu itakayoonyesha hali halisi ya zoezi hilo, athari za ugawaji wa vitambulisho katika vyanzo vya mapato, ushauri wa menejimenti na kupitia upya sheria za mapato za serikali za mitaa ili kuepuka hoja za ukaguzi na hati chafu.

Katika kikao hicho pia maazimio mbalimbali yaliweza kutolewa ikiwemo suala la kutenga bajeti za kata kwa ajili ya maboresho muhimu ya miundombinu ambapo Mkurugenzi wa jiji la Arusha Dkt. Maulid Suleiman Madeni amesema kwakuwa bajeti ya mwaka huu wa fedha ilishapitishwa hivyo amewaomba madiwani na maafisa watendaji wa kata kuwasilisha taarifa za maboresho ya miundombinu katika maeneo yao ya utawala kwa ajili ya kutengewa fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha ujao, 2019/2020.

Aidha kikao hicho cha baraza la Madiwani kilipokea  taarifa mbalimbali kutoka katika taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zinazotoa huduma kwa wananchi wa Jiji la Arusha.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa