• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

MAHAFALI YA PAMOJA YA KIDATO CHA NNE SHULE ZA SEKONDARI ZA JIJI LA ARUSHA

Posted on: October 26th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mh. Gabriel Daqarro amezungumza na wanafunzi wanaotarajiwa kuhitimu masomo yao ya kidato cha nne mwezi Novemba 2019 katika mahafali ya shule za sekondari za Jiji la Arusha  yaliyofanyika mapema leo Tarehe 26 Oktoba 2019 katika viwanja vya Shule ya sekondari Arusha. Mahafali haya yamehusisha shule za sekondari za Serikali na binafsi zilizopo Jijini Arusha.

Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli  ilitoa ahadi ya elimu bila malipo mwaka 2015 na imetekeleza ahadi hiyo hivi sasa wanaotarajiwa kuhitimu elimu ya kidato cha nne novemba mwaka 2019 ni zao la kwanza la elimu bila malipo.

Kwa mwaka 2016 wanafunzi waliohitimu elimu ya kidato cha nne Jijini Arusha walikuwa wanafunzi wapatao 4,447 bali hivi sasa wanaotarajiwa kuhitimu kidato cha nne mwaka 2019  wameongezeka paka kufikia wanafunzi 6,833 ikiwa ni ongezeko kubwa na hii ni kwasababu ya juhudi za Serikali ya awamu ya tano kutoa elimu bila malipo hivyo kupelekea wazazi wengi kupeleka watoto shule.

Akihutubia wanafunzi katika mahafali ya kidato cha nne Mh.Gabriel Daqarro amewaeleza wanafunzi hao kuwa hakuna namna mwanafunzi atajitenga na Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwani wote ni matunda yake na  amewawaomba wanafunzi hao kumrudishia Mh Rais zawadi ya ufaulu wa alama nzuri kwenye mitihani yao ya mwisho ikiwa ni ishara ya kuonyesha juhudi na matokeo chanya ya elimu bila malipo.

Pamoja na kuwahusia wanafunzi Mh. Daqarro amezungumza na walimu wa shule hizo zilizohudhuria mahafali hayo kwa kuwashukuru juu ya juhudi mbalimbali wanazoendelea kuzifanya ili kuleta matokeo chanya katika sekta ya elimu, juhudi hizo zikiwa ni pamija na utaratibu wa namna walivyoanzisha makambi ambayo wamewaweka wanafunzi kwaajili ya kujiandaa na mitihani. Amesema makambi hayo yamekuwa na matokea chanya kwani katika mitihani ya mock wanafunzi hao wamefanya vizuri na kupelekea Jiji la Arusha kuongoza kwa kushika nafasi ya kwanza katika mkoa wa Arusha.

Pamoja na hayo Mh. Daqarro ameeleza kuwa kutokana na changamoto ya upungufu wa chakula mashuleni kuonekana ikikithiri wazazi wahinizwe zaidi juu ya kuchangia chakula cha wanafunzi kwani waraka wa elimu unaelekeza kuwa chakula cha wanafunzi kitagharamiwa na wazazi.

Afisa Elimu Sekondari Jiji la Arusha Ndg. Valentine Makuka ameipongeza serikali ya chama cha mapinduzi chini ya Mh. Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuongeza vyumba vya madarasa kutokea vyumba 448 kwa mwaka 2016 paka kufikia vyumba 500 mwaka 2019. Pia ameishukuru Serikali kwa kuhakikisha adha ya meza na viti imetoweka na sasa kila mwanafunzi ana meza na kiti chake. Pamoja na pongezi hizo ameishukuru serikali juu ya fedha zinazotolewa za elimu bila malipo kwani mwaka 2016 zilikuwa ni 645,573,000 hadi kufikia mwaka 2019 zimeongezeka nakufikia 3,758,192,931.45   Pia ameshukuru ofisi ya mkurugenzi wa Jiji la Arusha kwa kutoa fedha na mbalimbali  kama motisha kwa walimu pamoja na kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo ambayo kwa sehemu kubwa yameleta matokeo chanya katika sekta ya elimu.

Aidha katika risala ya wanafunzi iliyoandaliwa na  kusomwa na mwanafunzi wa kidato cha nne Bi. Mwanaisha Mtwana wanafunzi wamemshukuru Mkuu wa Wilaya Daqarro kwa kuwa mdau mkubwa wa elimu hasa katika kufuatilia kwa ukaribu zaidi maswala ya elimu kuhakikisha kuwa taaluma katika Jiji la Arusha inaimarika na hasa lengo la kuondoa daraja sifuri katika ufaulu linatimia. Wakieleza changamoto zao wameiomba Serikali kuhimiza wazazi wachangie gharama za chakula mashuleni ili kusudi wanafunzi wote wapate utulivu wa akili darasani kwani mototo aliyeshiba anauwezo wa kujifunza na kuelewa vizuri.

Akihitimisha mahafali hayo Dc Daqarro amegawa vyeti kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani ya mock kidato cha nne mwaka 2019 ikiwa ni mwanafunzi mmoja bora kwa kila shule iliyofanya mitihani ya mock lakini pia amegawa vyeti kwa walimu ambao wamefanya vizuri katika masomo yao wanayofundisha hii ikiwa ni mwalimu ambae somo lake limekuwa na ufaulu mzuri kwenye mitihani ya Mock.

Pichani: Mh. Daqarro watatu kulia mstari wa mbele akiwa na wanafunzi wakiume waliotunukiwa vyeti vya ufaulu mzuri katika mitihani ya Mock kidato cha nne 2019


 Pichani: Mh. Daqarro watatu kulia mstari wa mbele akiwa na wanafunzi wakike waliotunukiwa vyeti vya ufaulu mzuri katika mitihani ya Mock kidato cha nne 2019


Pichani: Mh. Daqarro watatu kulia mstari wa mbele akiwa na walimu ambao wamefanya vizuri katika masomo yao wanayofundisha hii ikiwa ni mwalimu ambae somo lake limekuwa na ufaulu mzuri kwenye mitihani ya Mock 2019.



Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa