• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

RC Gambo, "Watumishi toeni ushirikiano kwa TRA katika zoezi la ukusanyaji wa mapato"

Posted on: September 3rd, 2018

Ametoa rai hiyo alipokuwa akiongea na watumishi wa Jiji la Arusha kufuatia agizo na msisitizo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Magufuli juu ya suala zima la ulipaji wa kodi na ukusanyaji wa  mapato kwa kuwa ndio  muhimili mkuwa wa Taifa letu.

Mkuu wa Mkoa pia katika kikao chake na watumishi wa Jiji la Arusha kilichofanyika hapo jana ameagiza watumishi kutoa ushirikiano kwa wakaguzi wa fedha wa ndani na nje  katika kuwasilisha taarifa muhimu za matumizi ili kukwepa hoja zisizo za msingi.

Pia miongoni mwa mambo aliyoyatilia msisitizo ni pamoja na suala la baadhi ya watumishi kutowabugudhi wafanyabiashara wadogo almaarufu kama machinga kama agizo la Rais linavyosema badala yake kama serikali tunawajibika kuwatengenezea mazingira rafiki na uhuru karika shughuli zao za kujiingizia kipato na sio kusimama kama kikwazo.

Kadhalika, aliwaonya mawakala wa ukusanyaji taka katika Jiji la Arusha kuacha kuwabugudhi wamiliki wa viwanda katika jiji hili kwa kukusanya tozo ama faini zisizo za lazima kwani wamiliki hao wa viwanda wamekuwa ni chachu ya kusogeza gurudumu la maendeleo katika jiji letu hivyo amewaagiza watumishi idara ya Usafishaji na Mazingira kulisimamia hilo.

“Kwa mfano mmiliki wa kiwanda cha Mount Meru Millers, mfanyabiashara huyu ni mdau mkubwa katika maendeleo ya elimu jijini hapa na amejitolea kufanikisha lishe ya kila siku kwa zaidi ya wanafunzi 20,000 kwa shule za msingi katika Jiji hili hivyo hapaswi kutozwa faini zisizo za kisheria na mawakala wachache wenye kutaka kuharibu sifa nzuri ya Jiji letu” alisema mkuu wa mkoa

Pia amewaagiza maafisa utumishi katika Halmashauri kutokuwa kikwazo kwa watumishi kupanda madaraja badala yake wasimamie maslahi ya watumishi ikiwemo kutatua changamoto ya upishanaji wa mishahara watumishi wanaopanda madaraja kwani kwa kutofanya hivyo kunashusha morali ya watumishi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Changamoto nyingine iliyobainishwa na Mkuu wa Mkoa huyo pia ni ukosefu wa matundu ya vyoo hasa katika shule za sekondari za kata ikiwemo shule ya Sekondari Mkonoo kata ya Terrat, mazingira ya vyoo vya walimu ni mabovu hivyo watumishi mnapaswa kulisimamia hilo na kutoa ushirikiano kwa wadau mbalimbali wanaojitokeza kutatua changamoto hizo.

Pia amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa Ndg. Richard Kwitega na  kushirikiana na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dr. Maulid Suleiman Madeni kutengeneza mpango mkakati kuhakikisha maeneo ya ardhi yanapimwa na wananchi kupatiwa hati miliki zao na watumishi wapewe kipaumbele katika kupatiwa viwanja vinayouzwa ikiwemo vya Mateves na Suye kwa  mikopo yenye riba nafuu.

“Katika upande wa afya  serikali inajenga vituo vikubwa vya afya katika jiji la arusha ikiwemo kituo cha afya Murret ambapo nichukue fursa hii kumpongeza Eng. Samuel Mshuza, Kaimu Mhandisi wa Jiji kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa kituo hicho. Pia tunajenga hospitali za wilaya kwa mkoa mzima ambapo kwa Jiji la Arusha ujenzi wa hospitali ya wilaya iliyopo katika kata ya Engutoto ipo katika hatua za umaliziaji” alisema Mkuu wa Mkoa.

Alimaliza kikao chake wa kuwahimiza watumishi kujiimarisha katika maandalizi ya Mwenge ambapo kwa Jiji la Arusha tunatarajia kuupokea Tarehe 18/09/2019  na ametilia mkazo upewe heshima inayostahiki.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa