• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Ubalozi wa China umekabidhi vifaa tiba katika kituo cha Afya Murriet Jijini Arusha

Posted on: February 19th, 2019

Ubalozi wa China nchini Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Gold Card Foundation ya nchini China umechangia  vifaa tiba katika kituo cha Afya Murriet kilichopo  Jijini Arusha, vifaa hivyo ni pamoja na kitanda cha upasuaji, mashine ya usingizi na taa maalum kwa ajili ya upasuaji.

Akiongea wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika leo tarehe 19 februari, 2019 mkuu wa Mkoa wa Arusha ametoa shukurani za kwa ubalozi wa China nchini Tanzania pamoja na kampuni ya gold card kwa kuchangia vifaa hivyo vitakavyosaidia uboreshaji wa huduma ya afya katika kituo hicho.

“katika kukabiliana na changamoto ya miundombinu katika eneo hili la murriet hasa kipindi cha masika, ujenzi wa barabara ya lami unaendelea  na wataalamu kutoka ofisi za Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini Tanzania (TARURA) wamehakikisha kukamilika kwake ndani ya mda mfupi ujao”  alisema Rc Gambo

“Kituo hiki kwa sasa hakina gari la kubebea wagonjwa, nataka niwatoe hofu wakazi wa Murriet na kata za pembezoni kuwa gari iko njiani na mda wowote kuanzia sasa linaweza kupokelewa na kwa mujibu wa mazungumzo niliyofanya na Balozi WAN KE kutoka ubalozi wa China nchini Tanzania ameahidi kuongeza vifaa vingine vyenye thamani ya shilingi Milioni 61.5 kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa huduma katika kituo hiki. Vifaa hivyo ni kama taa za chumba cha upasuaji, dawa za kuondolea usingizi na kitanda cha kufanyia upasuaji  wagonjwa”  alisema Mkuu wa Mkoa huyo.

Aidha Rc Gambo alitoa pendekezo la kuenzi jina la Mama Hadija kwa kuifanya wodi mojawapo katika kituo hicho kuwa na jina lake kwa ajili ya kumshukuru kwa moyo wake wa kizalendo na utu wake kwani kupitia yeye kutoa kiwanja chake ndipo wazo la kujenga kituo hicho cha afya likapatikana.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Mhe. Gabriel Daqarro ametolea ufafanuzi nguvu kubwa inayotumika katika kuboresha kituo hicho kuwa ni kutokana na kata hiyo kuwa pembezoni mwa mji na kuwa na idadi kubwa ya watu kutoka katika kata hiyo na kata za jirani.

“Napenda kuishukuru serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha Shilingi 700,000,000.00  kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki kwani tangu kianze kutoa huduma kimekuwa kikipunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali za mjini”

Naye GAO WEI , Mwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania  amesema kuwa yeye na wawakilishi wenzie wa taasisi hiyo ni mara yao ya kwanza kufika Tanzania hivyo wamefurahia ukarimu wa Watanzania na hali ya hewa nzuri iliyopo Jijini Arusha na wataendelea kusaidia uboreshaji wa  huduma za kijamii ili kuboresha mahusiano mazuri na urafiki wa nchi ya China na Tanzania.

“UDUMU URAFIKI WA CHINA NA TANZANIA”

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa