• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa 10 Jimbo la Arusha mjini watangazwa,vyama vyajitokeza kushiriki

Posted on: May 7th, 2021

Uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa 10 Jimbo la Arusha mjini watangazwa,vyama vyajitokeza kushiriki

Na Mwandishi wetu

MSIMAMIZI wa uchaguzi wa Jimbo la Arusha mjini ambaye pia ni Mkurugenzi wa Jiji la Arusha  Dk.John Pima ametangaza tarehe ya uchaguzi wa Wenyeviti wa mitaa 10 ambayo iko wazi baada ya wenyeviti wa mitaa hiyo kuchaguliwa kuwa Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha  na wengine kufariki dunia. 

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari  Dk.Pima alisema kuwa waliokuwa  wenyeviti wa mitaa wapatao nane (8) waligombea nafasi ya udiwani  na kushinda na hivyo nafasi zao kuwa wazi  na wenyeti wawili walifariki dunia na kwamba nafasi hizo ziko wazi kwamba uchaguzi wa kujaza nafasi hizo utafanyika Julai Mosi  mwaka 2021. 

Alisema kuwa   wenyeviti hao walichaguliwa mwaka 2019 na kuwa baada ya nafasi kuwa wazi sheria haina budi kufutwa na kwamba sheria ya serikali za mitaa kifungu  44 (1) (2) inaeleza bayana kuwa nafasi zikiwa wazi lazima uchaguzi urudiwe  kujaza nafasi hizo. 

Alitaja mitaa hiyo kuwa ni  mtaa wa Goliondoi  kata ya Sekei, Olmatejo B kata ya Sakina, Kwa mrefu kata ya Baraa ,Kirika B kata ya Osunyai JR. 

Nyingine ni Olkung’u na Erangau kata ya Terrat, Darajani kata ya Ungalimited, Saccon kata ya Elerai, Block C kata ya Engutoto na Olmokeo kata ya Sinoni .

Dk.Pima anasema kuwa uchaguzi huo ni kwa mujibu wa kifungu cha 9 cha  kanuni za uchaguzi za wenyeviti   wa mitaa  na wajumbe wa kamati za mtaa katika mamlaka ya  wa serikali za mitaa  ambapo kifungu  hicho kinamtaka Msimamizi wa uchaguzi kutangaza siku 62 uchaguzi huo  kabla ya tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo. 

Dk.Pima anafafanua kuwa  tarehe 10 Mei 2021 wateteuliwa  maafisa ambao watasimamia zoezi zima la kuandaa  orodha ya wapiga kura  katika maeneo ya mitaa 10  na wataapishwa tarehe  11 na tarehe 12 Mei  2021 watafanyiwa  mafunzo ya namna ya kusimamia uchaguzi huo. 

Alisema zoezi la uandikishwaji katika daftari la kupiga kura litaanza mara ya mafunzo ya maafisa na uandikishwaji utakuwa unafanyika kila siku kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni  na itaanza mwezi Mei, 202. 

“Wapiga kura ni wakazi wa mtaa husika na watakiwa wawe na sifa zifuatazo, awe ni Raia wa Tanzania Tanzania , awe miaka  wa miaka 18 na zaidi  awe hana ugonjwa  wa akili, awe amejiandikisha kupiga kura na zoezi la uandikishaji na kupiga kura litafanyika katika  maeneo ya vituo vilivyotumika mwaka 2019 katika uchaguzi huo. “anasema Dk.Pima. 

Dk.Pima anasema tayari vyama  11  vimejitokeza kushiriki uchaguzi huo na kwamba  matangazo yataendelea kutolewa kuhamasisha watu wenye nia ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa mtaa kujitokeza ikiwa ni haki ya msingi ya kila mtu. 

Pamoja na mambo mengine  alieleza Sifa za wagombea kuwa ni  awe na umri wa miaka  21 au zaidi na uwezo wa kusoma na kuandika, awe na shughuli  inayomuwezesha kuendesha maisha, awe amedhaminiwa na chama husika na awe  pia ni mwanachama wa chama anachogombea nafasi hiyo na awe mwanachama na amedhaminiwa na chama hicho husika, awe hana kosa la jinai. 

Aliwataka wagombea na Viongozi wa Vyama vya Siasa kuwa mabalozi wa amani katika maeneo yao hatimaye uchaguzi huo uweze kufanikiwa na kuwapatia wananchi kuchagua viongozi wanaowataka. 

Awali Mkuu wa Wilaya ya Arusha Kenan Kihongosi aliwahakikishia viongozi wa kisiasa na wananchi kuwa uchaguzi utafanyika kwa amani ambapo amewataka Viongozi wa kisiasa kuepuka lugha za matusi na kashfa wakati wa kampeni  kuelekea uchaguzi huo. 

Mh.Kenan aliwataka viongozi wa kisiasa kuwa mstari wa mbele kulinda amani kwa kuhakikisha kuwa kampeni zinafanyika kwa ustaarabu bila kuharibiana na kuvunjiana heshima miongoni mwa wagombea. 


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa