• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Viongozi Halmashauri ya Jiji la Arusha waahidi utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Posted on: September 9th, 2021

Na Mwandishi wetu.

Madiwani na Wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wamedhamiria kuhakikisha wanashirikiana kwa umoja wao kusimamia utekelezaji wa miradi kwa ufanisi na kwa wakati na hatimaye kuweza kuwaletea maendeleo zaidi wananchi wa Jiji hilo.

Hayo yamesemwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Mhe. Maxmillian Iranqhe mara baada ya kumalizika kwa Baraza la Madiwani la robo ya nne ya mwaka lililofanyika siku ya Alhamisi katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Mhe. Iranqhe alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ilifanikiwa kukusanya zaidi ya Shillingi billioni 17.7 ambayo ni sawa na asilimia 80 ya vyanzo vyote vya makusanyo ya ndani ambapo kiasi cha zaidi ya Shillingi billioni 9.3 ziliweza kutumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Jiji la Arusha zikiwa ni fedha za mapato ya ndani, Ruzuku kutoka Serikali kuu na Wafadhili mbalimbali.

Mhe. Iranqhe alisema kuwa kuelekea mwaka wa fedha 2021/2022 viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wataendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato mengi ili fedha hizo ziende kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba wamejipanga kuhakikisha utekelezaji wa miradi unafanyika kwa ufanisi na kwa wakati.

Aidha Mhe. Iranqhe amesema kwamba katika kipindi cha mwaka huu wa fedha Halmashauri inategemea kukusanya kiasi cha zaidi ya Sh. Bil. 24 kufanikisha utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za Msingi na Sekondari, matundu ya choo, ujenzi wa jengo jipya la Utawala la Halmashauri, barabara, vituo vya afya na miradi mingineyo mingi ya maendeleo.

"kwa mwaka huu fedha tunategemea kukusanya zaidi ya shilingi Bil. 24 na pesa hizo zikipatikana asilimia zaidi ya 60 zinaenda kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikiwemo Ujenzi wa jengo jipya lenye hadhi la Utawala la Halmashauri, na kwa upande wa elimu ya Msingi tumepanga kujenga madarasa 50, Elimu Sekondari madarasa 50, matundu ya choo zaidi ya 70, vyote hivi kupitia mapato yetu ya ndani" alisema Mstahiki Meya.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha Dk. John Pima alisema kuwa kwa mwaka wa fedha uliopita wa fedha 2020/2021 moja ya maeneo ambayo Halmashauri ya Jiji la imefanya vizuri ni kwenye mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wakina mama na watu wenye ulemavu ambapo jumla ya mikopo yenye thamani ya Sh. bilioni 2.17 ilitolewa.

Ameongeza kwa kusema kuwa jumla ya mikopo yenye thamani Sh. Billioni 1.19 imetolewa kwa vikundi 88 vya wakina mama, mikopo yenye thamani ya Sh. Milioni 895.7 imetolewa kwa vikundi 51 kwa vijana, na walemavu mikopo yenye thamani ya Sh. million 82.8 imetolewa kwa vikundi 9.

Dk. Pima alimalizia kwa kuwapongeza wananchi kwa kuwa ni fedha walizochangia na nyingine zimerejeshwa, akiongeza kuwa Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa mwaka huu wa fedha itaendelea kutoa mikopo hiyo huku akihimiza makundi lengwa kujitokeza kwa wingi kuchukua mikopo hiyo ili kujikwamua kiuchumi.


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa