• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

WAKUU wa Shule za Sekondari Jiji la Arusha wapongezwa ,Watakiwa kukataa Sifuri katika Shule zao

Posted on: July 12th, 2021

Na Mwandishi wetu

WAKUU wa Sekondari katika Jiji la Arusha wamepongezwa kwa kuwezesha wanafunzi wa kidato cha Sita kufanya vizuri katika mitihani yao na kwamba hiyo ni dalili tosha kuwa Shule za Sekondari za Serikali  katika Jiji hilo zinaweza kufanya vizuri na kufuta sifuri kwa wanafunzi wanaosoma katika shule zao. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dk.John Pima wakati akizungumza na Walimu wakuu wa Shule za Sekondari wa Jiji la Arusha katika ukumbi wa mikutano ya Jiji la Arusha. 

Dk.Pima alisema kuwa anawapongeza walimu na timu nzima ilijihusisha kusimamia mitihani hatimaye kuwezesha wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao. 

Anasema kuwa pamoja na kuwa wamefanya vizuri bado wanajukumu la kuhakikisha kufanya vizuri zaidi kwa kufaulisha kwa madaraja ya juu. 

“Unajua hizi shule zetu sita zinaweza kuwa katika kumi bora, inawezekana kabisa ni jitihada zinahitajika, kwani wanaufaulu wananini na sisi tunashindwa nini ?” anasema Dk.Pima

Pima alisema kuwa juhudi zaidi zinahitajika za kuhakikisha kila mwanafunzi anafanya vizuri na kuwafuatilia kwa karibu wanafunzi ambao wanadhaniwa kuwa na changamoto ikiwa ni kubaini namna yakuwasiadia waweze kufanya vizuri. 

Dk. Pima aliaagiza walimu waliofanya vizuri kupatiwa zawadi ya fedha kwa kufanya vizuri na kutaka agizo hilo kutekelezwa  mapema. 

Afisa Elimu Sekondari Valentine Makuka akitoa ufafanuzi wa mtokeo ya kidato cha sita alisema kuwa  jumla ya  wanafunzi waliopata daraja la kwanza  56, Daraja la Pili  wanafunzi  295  Daraja la tatu, 198   na daraja la Nne wanafunzi   8 na zero  2 ikiwa ni matokeo ya shule sita. 

Bw. Makuka alisema kuwa wanafunzi hao ni kutoka shule sekondari Sita na kuwa wanafunzi waliopata daraja la mwisho walikuwa na changamoto ya kitaaluma na wengine walikuwa wagonjwa. 

“Niseme kuwa baadhi ya wanafunzi walikuwa wagonjwa na wengine ni changamoto ya taaluma ila tunaahidi kufuta zero na Four kwa kuwa tunaweza .”

Makuka  alisema kuwa wanauwezo wakufanya vizuri na kwamba tayari wameanza kujipanga kufikia nia njema ya kufanya vizuri kitaaluma ikiwa ni pamoja nakuingia katika kumi bora. 

Naye Afisa Elimu Msingi Omary Kwesiga akizungumza na walimu hao aliwahikikishia kuwa wanauwezo wa kufanya vizuri kama ilivyo katika shule za Msingi na kwamba wanahitaji kubuni mbinu bora za kufundisha wanafunzi na kuwa karibu na wanafunzi ambao wanadhani wana changamoto katika ufaulu wao. 

Pamoja na mambo mengine aliwataka kuwa na ushirikiano pamoja na malengo yakufanya vizuri kwa kufuata ufuatiliaji wa karibu ikiwa ni kuweza kubaini ni wapi wanafunzi wanakwama katika taaluma kabla yakufikia katika mitihani yao ya mwisho ya kuhitimu kidato husika.


 

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa