• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Wanafunzi na wasomi wa Chuo cha Uhasibu kukabiliana na ukosefu wa ajira, waomba Serikali na wadau kuwatafutia soko la bidhaa zao

Posted on: April 23rd, 2021

Wanafunzi na wasomi wa Chuo cha Uhasibu kukabiliana na ukosefu wa  ajira, waomba Serikali na wadau kuwatafutia soko la bidhaa zao.

Na Mwandishi Wetu

KATIKA kukabiliana na changamoto ya ajira Uongozi wa Chuo cha Uhasibu kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wameanza kuwajengea uwezo Vijana na wasomi wa Chuo hicho wa kuanzisha shughuli za ujasirimali kwa kutumia vipaji walivyonavyo pamoja na kundeleza ubunifu waliona kwa kutumia teknolojia za kisasa na vitu vya asili. 

Vijana mbali na kupata elimu ya darasani wanapata muda wa kujifunza na kuonyesha vipaji vyao pamoja na kuzalisha bidhaa bora ambazo zinawaingizia kipato. 

Vijana hao wanatarajia mara baada ya kumaliza masomo yao kujiajiri na kuajiri vijana wenzao kwakuwa tayari wamepikwa na kupewa elimu sahihi ya ujasirimali. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wakionyesha bidhaa wanazozalisha kwa Mgeni Rasmi katika siku ya kuendeleza vipaji  ambayo Mgeni rasmi ni Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dk.John Pima wanasema kuwa wanajiona wenye bahati kwa kupata elimu ya kujitegemea na kuomba wadau wa maendeleo kuunga kazi zao mkono kwa kuwatafutia soko sahihi la bidhaa zao. 

Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo cha Uhasibu Sunday Cuthbeth Masawe akishukuru kwa niaba ya wanafunzi wenzake wabunifu aliomba Serikali na wadau kuunga mkono jitihada za Vijana hao wabunifu kwa kuwatafutia masoko pamoja na kuwapatia fursa za kutoa elimu ya ugunduzi, vipaji na ubunifu lengo ikiwa ni kuibua Vijana wenye vipaji kama hivyo.

Kaimu Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Gloria Kimburu akimkaribisha mgeni Rasmi kuzungumza na wanafunzi hao mara baada ya kutembelea na kuona kazi za wanafunzi wasomi wa Chuoni hapo  alisema kuwa Chuo hicho kina nia njema ya kuwajengea uwezo vijana hao kwa kuendeleza vipaji vyao na hatimaye kuondokana na tatizo la Ajira pindi watakapomaliza masomo yao. 

Bi Kimburu Alisema maarifa na ujuzi  ni jambo muhimu sana kwa Vijana na kwamba yatawasaidia kukabiliana na dunia ya Sayansi na Teknolojia .

Pamoja na mambo mengine ameiomba Serikali na wadau wa maendeleo kuhamasisha elimu ya kujitegemea ikiwa na lengo la kuibua vipaji kwa vijana na kupunguza wimbi la vijana ambao hawana ajira. 

 Mgeni Rasmi  katika siku ya ubunifu na  Vipaji (Carrer Day)  Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dk. John Pima alisema kuwa Serikali inatambua juhudi  za Vijana hao na kwamba Jiji la Arusha lina fursa lukuki za uwekezaji na kuwataka kutembelea Jiji hilo vivutio vilivyopo  na kuwekeza  na kwamba Vijana wanapewa kipaumbele ikiwa watakuwa tayari kuanzisha shughuli za ujasirimali wenye tija. 

Dk. Pima anawakumbusha vijana kuhusu uzalendo na kupenda nchi yao na kwamba Taifa linajengwa na vijana wazalendo  kuwa njia mojawapo ni kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali na kujipatia kipato badala  ya kulalamika  kuwa hakuna  ajira. 

Anawambia Vijana hao kuwa zipo  fursa nyingi katika Jiji la Arusha kama vile mojawapo ikiwa ni fursa ya Utalii.

‘’Arusha ni kitovu cha utalii chenye vivutio leteni mawazo na kuandika mipango kazi yenu ikiwa inafaa tutawapatia ushirikiano muweze kuwekeza tuna raslimali nyinyi za uwekezaji" alisema Dk. Pima. 


Pichani: Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dk. John Pima alipokutana na kuzungumza na wasomi wa Chuo cha Uhasibu Jijini Arusha katika siku ya kuonesha ubunifu na vipaji vyao (Career Day) na kupata fursa ya kujionea bidhaa ambazo ni zao la vijana hao wabunifu. 


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa