• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Wananchi Jijini Arusha watakiwa kujenga tabia ya kufanya usafi mara kwa mara

Posted on: September 17th, 2022

Mwandishi wetu 

BALOZI wa Rwanda nchini Tanzania Meja Jenerali, Charles Karamba amewaomba wananchi wa Jiji la Arusha kujenga tabia ya kufanya usafi wa mazingira yao,mara kwa mara ili kuvutia watalii na kuweka taswira nzuri  ya nchi kimataifa.

Akizungumza leo Jijini Arusha wakati aliposhirikia shughuli ya usafi,katika eneo la soko kuu na stendi kuu ya mabasi,Meja Jenerali Karamba alisema usafi huweka taswira ya nchi vizuri duniani na kuvutia wengi.

"Wananchi jengeni Tabia ya kufanya usafi mara kwa mara, ukiangalia Arusha ni kitovu cha utalii,hii itasaidia kuweka taswira nzuri ya nchi kimataifa na usafi huepusha  uzalishaji wa wadudu wanaoleta magonjwa ya mlipuko,"alisema.

Pia, alisema usafi licha ya kuweka taswira ya nchi vizuri duniani,lakini unasaidia kupunguzia serikali gharama ya kuondoa taka, kwa sababu hakutakuwa na taka nyingi zilizorundikana za kuziondoa.

Aidha, alisema nchini Rwanda wamezoea kufanya usafi kila Ijumaa na mwisho wa mwezi kushiriki na viongozi wao katika shughuli hiyo.

"Kila mmoja anapenda mazingira safi,tukiweka mazingira yetu safi  watalii watavutiwa zaidi na kutangaza kwao sifa ya usafi,hivyo tusiache kufanya usafi na sisi tupo tayari kushirikiana katika hili,"alisisitiza.

Alipongeza uwepo wa mahusiano mazuri baina ya nchi hizo na kuwasihi wananchi kushikamana na viongozi wao kwenye mazuri wanayowaelekeza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha Saidi Mtanda alishukuru  Wanyarwanda, kushiriki katika shughuli ya usafi ambao umefanyika katika kiwango cha kuridhisha.

"Serikali katika kuhakikisha Jiji hili linaendelea kua safi na la kimataifa ukizingatia jiji la kitali, imetoa zaidi ya Sh bilioni 40 kwa ajili ya kujenga soko la kimataifa eneo la Bondeni City na mwezi ujao tenda itatangazwa, ili apatikane mkandarasi na ujenzi uanze,"alisema.

Alisema sambamba na ujenzi huo barabara za lami, soko la Kilombero,Murombo na la machinga katika eneo la stendi hiyo yatajengwa kwa kutumia fedha zaidi ya Sh.bilioni 100 zilizotengwa za mradi wote huo.

Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Maximilian alisema Arusha ni lango la utalii kwa sababu watalii wengi wanaofikia nchini hupitia Arusha kwenda kwenye hifadhi mbalimbali,hivyo kujenga tabia ya kufanya usafi kitaipaisha kimataifa mkoa huo.


Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Maximilian alisema Arusha ni lango la utalii kwa sababu watalii wengi wanaofikia nchini hupitia Arusha kwenda kwenye hifadhi mbalimbali,hivyo kujenga tabia ya kufanya usafi kitaipaisha kimataifa mkoa huo.



Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Hargeney Chitukuro aliwashukuru wananchi kujitokeza kwa wingi, kushirikiana na Balozi huyo kufanya usafi na kuwaomba kuendeleza tabia hiyo na kukemea watakaowaona wakitupa taka hovyo. 

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa