• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

WAZAZI NA WALIMU WAELIMISHENI VIJANA KUHUSU UKIMWI

Posted on: December 1st, 2023

Katibu Tawala Wilaya ya Arusha Kamala Simba amewataka wazazi na walimu kuwa karibu na watoto wao kwa kuwashauri na kuwaelimisha dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI na Magonjwa yasiyoambukizwa.

Ametoa wito huo alipokuwa akizungumza na wananchi wa  Wilaya ya Arusha kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo Felician Mtahengerwa katika maadhimisho ya kilele cha siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika katika stendi ya Kilombero.

" Kundi lilikopo kwenye hatari zaidi yakupata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ni vijana katika umri balee hivyo wazazi na walimu mkae nao karibu katika kuwashauri na kuwapa elimu".

Kamala amewahamasisha wananchi wa Wilaya ya Arusha kwenda kwenye vituo takribani 24 vya afya vinavyotoa huduma ya kupima VVU ,pia wajawazito wajitokeze kwenye vituo 60 vinayotoa huduma ya Mama na Mtoto katika Wilaya ya Arusha.

Hali ya upimaji katika Wilaya ya Arusha imeshuka kutoka asilimia 3.1 mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 2.3 mwaka 2022 na hali ya maambukizi kwa Mkoa wa Arusha ni asilimia 1.9, hivyo wananchi wametakiwa kutoridhishwa na hali hiyo bali waendelee kujitokeza kwa wingi kupima afya zao.

Lengo la Serikali ni kutokomeza UKIMWI ikifika mwaka 2030, hivyo ili kufikia lengo hilo jamii inatakiwa kujitokeza kupima kwa wingi na watakao gundulika wanamaambukizi wanatakiwa kuanza kutumia dozi ya dawa mapema.

Aidha, amesema Serikali itaendelea  kuviwezesha vikundi vya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kwa kuvipatia Mikopo ya Asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Arusha ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Sambamba na hilo bado juhudi za Serikali zimeendelea kuonekana kwa Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa  kulipia gharama za matibabu kwa watu wanaoishi na VVU  100 sawa na kaya 20 pamoja na watu 175 wenye uraibu kwa mwaka 2022/2023.

Vilevile, katika kilele cha maadhimisho hayo Halmashauri imetoa kadi za Bima ya afya (iCHF) 210  yenye thamani za zaidi ya milioni 1 kwa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI sawa na kaya 35.

Pia, amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na watendaji wa Vijiji kutofumbia Macho vitendo vya ukali wa kijinsia ambavyo vimeonekana ni chanzo kimoja wapo cha maambukizi ya VVU katika jamii.

Amesema, maadhimisho hayo ya siku ya UKIMWI Duniani yapo ndani ya siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia yaliyoanza Novemba 25 na yatahitimishwa Disemba 10,2023.

Kwa upande wake, Mratibu wa kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Arusha Rosemary Tigano, amesema katika   maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniania Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wameweza kutoa elimu kwa vijana zaidi ya 798 wa vyuo vikuu navya kati, wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari,Madereva Bodaboda, wafanyabiashara wa masoko, mafundi ujenzi, viongozi wa dini,wateja wa vilabu vya pombe za kienyeji katika kata ya Ngarenaro na Kaloleni.

Amesema jumla ya Kondom 13,791 ziligawiwa na wananchi 343 walifanyiwa uchunguzi na kati yao 194 walipimwa  na 3 walibainika kuwa na maambukizi ya VVU na watu hao wameshaunganishwa na huduma za tiba na matunzo.

Maadhimisho hayo yaliambatana na utoaji wa huduma mbalimbali zikiwemo;Upimaji wa Sukari, Shinikizo la Damu,Uzito,Saratani ya Mlango wa Kizazi,Saratani ya tezu Dume zilizoambatana na utoaji elimu na ushauri wa Kitaalamu.

Halmashauri ya Jiji la Arusha limeadhimisha siku ya UKIMWI Duniani kwa siku 3 kuanzia Novemba 29 hadi kilele chake Disemba 1,2023 sambamba na kauli mbiu isemayo " Jamii iongeze Kutokomeza UKIMWI".



Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa