• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

WAZIRI JENISTER AWATAKA VIONGOZI NA WATENDAJI SERIKALINI KUSIMAMIA KIKAMILIFU RASILIMALIWATU

Posted on: October 10th, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amewataka Viongozi na Watendaji katika taasisi za umma kusimamia kikamilifu rasilimaliwatu ili kuepusha migogoro sehemu za kazi kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Jenista amesema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Arusha, Jiji na Halmashauri ya Wilaya ya Arusha wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji na kutatua kero na changamoto zinazowakabili watumishi wa umma mkoani humo.

Mhe. Jenista amesema migogoro katika sehemu za kazi mara nyingi inatokana na watumishi wa umma kutotendewa haki katika kupatiwa stahiki zao, hivyo ni wajibu wa viongozi na watendaji kusimamia rasilimaliwatu hii kikamilifu ili kuepusha migogoro hiyo ambayo sio ya lazima katika sehemu hizo za kazi.

“Viongozi na watendaji waliopewa madaraka ya kuhakikisha eneo la kazi linakuwa salama, lenye amani, utulivu na lenye kuleta tija kwa taifa wakitimiza majukumu yao ipasavyo, migogoro mingi sehemu za kazi haitakuwepo na kila mtumishi atafurahia kufanya kazi katika eneo lake.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa hakuna sababu ya kuwafanya watumishi wakate tamaa na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa kuwanyima haki zao za msingi.

Amesema ni wakati sasa wa viongozi na watendaji wa taasisi za serikali kuiga kwa vitendo yale yote yanayofanywa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wa ngazi za juu katika kuliletea taifa maendeleo.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anaongoza kwa vitendo, hivyo ni wakati sasa wa kubadilika, tuuvae uzalendo anaoudhihirisha Rais wetu kwa vitendo, kila mmoja ajisikie anadaiwa kutekeleza wajibu wake na anayeishi kwa kuwanyanyasa anaowaongoza aache mara moja kwani ni dhambi kubwa,” Mhe. Jenista amesisitiza.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa, watumishi wa umma wanapatikana kwa kuzingatia uwezo walionao na kwa kuwapanga kwa lengo la kujenga uchumi wa taifa na kuleta maendeleo endelevu, hivyo hawatakiwi kukutana na vikwazo vinavyowakatisha tamaa bali wakutane na mazingira wezeshi yanayowapa ari na kusonga mbele katika kutekeleza majukumu yao.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa, mchango mzuri unaotolewa na watumishi wa umma katika kuliletea taifa maendeleo unatambulika na viongozi wa ngazi za juu akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na ndio sababu ametoa kipaumbele kwa watumishi wa umma kupatiwa stahiki zao kwa wakati.


“Dira na maono ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ni kuwa na utumishi wa umma wenye kuleta tija kwa taifa na ndio maana amekuwa akijali masilahi ya watumishi ili kufikia malengo yake akiamini bila rasilimaliwatu yenye ubora basi rasilimali nyingine haziwezi kutekelezeka, hivyo ni wajibu wa viongozi na watendaji kusimamia masilahi ya watumishi kama ambavyo Mhe Rais ameleekeza.” Mhe. Jenista amesisitiza.

Mhe. Jenista ameanza ziara ya kikazi ya siku tano ya mkoani Arusha yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji na kutatua kero na changamoto zinazowakabili watumishi wa umma pamoja na kukagua utekelezaji wa miradi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge (MKURABITA).


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa