• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Asilimia 96 ya watoto Jijini Arusha wafikiwa na huduma ya mwezi wa afya na lishe ya mtoto

Posted on: October 19th, 2018

Takwimu hiyo imetolewa na Afisa Lishe Jiji la Arusha Bi. Rose Mauya alipokuwa akitoa taarifa ya  utekelezaji wa majukumu ya kitengo cha lishe wakati wa kikao cha robo ya  kwanza  ya mwaka wa fedha 2018/2019 kilichojumuisha wajumbe wa kamati za lishe ngazi ya Wilaya .

Katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Arusha jana Tarehe 18, Otoba 2018, Bi. Rose ameyaelezea mafanikio  ya shughuli za lishe  kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kuwa ni pamoja na  wazazi  na  walezi 20, 543  wamenufaika na    utolewaji wa elimu kuhusiana na mwezi wa lishe ya mtoto iliyotolewa katika vituo vyenye huduma ya mama na mtoto  ambapo ilihusisha utoaji wa matone ya Vitamin A, utoaji wa vidonge vya kuondoa maambukizi ya minyoo na ufanyaji wa tathmini ya hali ya afya ya lishe.

Mafanikio mengine ni utolewaji wa elimu ya lishe kuhusiana na mlo kamili, mtindo bora wa maisha na magonjwa yasiyoambukiza  kwa vikundi vya vijana na wanawake wakati wa mafunzo ya utolewaji wa mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali ambapo zaidi ya watu 156 walipatiwa elimu hiyo.

“Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 watoto waliokuwa na hali mbaya kilishe waliweza kubainika na kupatiwa huduma, sambamba na kuhakikisha wazalishaji wa bidhaa za vyakula wanazingatia umuhimu wa urutubishaji wa vyakula” aliongeza Bi. Rose

Naye mganga mkuu wa jiji la arusha ambaye ndiye katibu wa kamati ya  lishe katika ngazi ya halmashauri Dr. Simon Chacha  ameyaelezea  maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji katika  kipindi cha July – Septemba kwa mwaka huu wa fedha tulionao  ambapo amesema kuwa maadhimisho hayo  yalifanyika katika vituo vya kutolea huduma za afya na viwanja vya Nanenane  ambapo ulifanyika upimaji wa hali ya afya kilishe na ufuatiliaji wa ukuaji wa watoto chini ya umri wa miaka mitano .

“Katika maadhimishi ya wiki ya unyonyeshaji tuliweza kutoa elimu ya unyonyeshaji kwa miezi 6 ya mwanzo kwa wazazi na walezi  ambapo jumla ya wazazi na lezi wenye watoto wa umri wa miezi 0-6 waliopatiwa elimu hiyo  ni 1,455, wazazi na walezi wenye watoto wa umri wa miezi 6-23 ni 2,235 na  wazazi na walezi wenye watoto wa umri wa zaidi ya miezi 23 – 2,892” alisema Dr. Chacha.

Dr. Chacha aliongeza kwa kusema kuwa miongoni mwa jukumu kubwa la kamati ya lishe Jiji la Arusha ni kuendelea kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa lishe bora, kuelimisha wazalishaji waweze kujua madhara ya kutofanya urutubisaji wa vyakula  na kufanya tathmini ya hali ya afya ya lishe pamoja na kuendelea kuwaelimisha wazazi na walezi juu ya umuhimu wa mwezi wa afya na lishe ya mtoto.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa