• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Halmashauri ya Jiji la Arusha yajipanga kukabiliana na magonjwa ya mlipuko.

Posted on: May 5th, 2023

Na Mwandishi Wetu 

Arusha. 

Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha imejipanga kuhakikisha inachukuwa tahadhari ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko katika kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha ambaye pia ni Mwenyekiti  wa Kamati ya Afya ya Msingi Msingi Wilayani humo, Mhe. Felician Mtahengerwa akizungumza katika kikao kazi cha robo ya mwaka cha kutathimini hali ya magonjwa ya milipuko kilichofanyika leo Mei 05,2023 Kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mkuu huyo wa Wilaya, ambapo amesema mvua hizi ni chanzo kikubwa katika kusababisha magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na mengineyo. 

"Sisi kama viongozi na sisi kama kamati tuna wajibu na kulazimika kujadili namna gani tutaweza kukabiliana na magonjwa haya ya mlipuko hivyo ni lazima tujiweke katika tahadhari linapotokea jambo tuwe katika namna nzuri ya kukabiliana nalo."alisisitiza Mtahengerwa . 

Aidha Mhe. Mtahengerwa amewaagiza Maafisa Afya wa kila kata kuwepo na maeneo ya wazi ambayo yatatumika kuwahifadhi wahanga wa magonjwa ya mlipuko endapo idadi yao itakuwa kubwa ambapo amewaomba wadau mbalimbali kuunga mkono jitihada hizo.

Ameongeza kwa kuwataka viongozi wa masoko kuweka vitakasa mikono katika maeneo yao na katika maeneo yenye misongamano ya watu wengi sambamba na kutoa elimu ya usafi wa mazingira kwa jamii.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha na Katibu wa Kamati ya Afya ya Msingi, Hargeney Chitukuro amesisitiza kuwepo kwa usafishaji wa mazingira katika maeneo yenye vyombo vya kuwekea takataka.

Aidha, Chitukuro ameelekeza kusambazwa kwa barua katika Taasisi za Dini zinazoelekeza uchukuaji wa tahadhari ambapo amewataka Maafisa Afya kupiga marufuku uuzwaji wa matunda yaliyokatwa pamoja na wale wanaouza vyakula waziwazi kwa usalama wa afya za wananchi.


Kwa upande wake Mwenyekiti Kamati ya Afya ya Msingi (PHC)B.Hindu Ali Mbwego ameiomba Mamlaka ya Maji Safi na Usafishaji wa Mazingira Jiji la Arusha(AUWSA) kuweka utaratibu wa kuyatibu maji angalau mara moja kwa wiki ili kuwakinga WATU dhidi ya magonjwa ya mlipuko hususani wanafunzi mashuleni.

Pamoja na hayo Bi.Hindu ameliomba jeshi la polisi kudhibiti na kutokomeza upikwaji na uuzwaji wa pombe za kienyeji ambazo kuchangia kwa kiasi kikubwa watu hususani vijana kupoteza maisha.


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa