• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Jaffo, “Kituo cha afya cha Murriet ndio kituo pekee cha mfano kati ya vituo 350 vipya vya afya vinavyojengwa hapa Nchini”

Posted on: November 9th, 2018

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jaffo (MB) amesema kuwa kituo cha Afya Murriet kilichopo katika kata ya Murriet Jijini Arusha ndio kituo pekee cha mfano kati ya vituo 350 vipya vya afya vinavyojengwa hapa nchini.

Waziri Jaffo ameyasema hayo wakati wa ziara yake Jijini Arusha leo Tarehe 09/11/2018 alipotembela  kituo hicho cha afya kilichoanza kutoa huduma kwa wananchi mwanzoni mwa juma hili pamoja na kukagua mendeleo ya ukarabati na ujenzi  wa baadhi ya majengo katika kituo cha afya Kaloleni ulioanza Tarehe 19/09/2018 kama alivyoelekeza wakati wa ziara yake aliyoifanya mwezi  Septemba mwaka huu.

Pia ametoa rai kwa waganga wafawidhi  wa vituo vipya nchini kuhakikisha wanaboresha mazingira kwa kutengeneza  bustani zitakazowezesha vituo kuwa na mandhari ya kupendeza na kuwawezesha  wananchi kuona kama hospitali ni sehemu ya utalii.

"Nawapongeza viongozi wa Mkoa wa Arusha akiwemo Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya , Mkurugenzi , Mganga Mkuu, mhandisi wa Jiji  na wengine kwa kusimamia vyema kazi za ujenzi wa vituo vya afya na hiki Kituo cha Murriet ni mfano mzuri. Na kwa hapa nchini tayari vituo vya afya vipya 210 vimekamilika katika miezi 18 na vingine vinajengwa na kufikia idadi ya 350 hivyo nilishaomba  Bohari ya Dawa (MSD) kuhakikisha wanapeleka dawa kwa wakati katika vituo vya afya " alisema  Waziri Jaffo

Pia amemuagiza Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Murriet, Bw. Mustafa Miraji kuhakikisha upatikanaji wa dawa kwa wananchi usiwe kikwazo na kamwe kusitokee malalamiko  kwa wananchi kuhusu utoaji wa huduma bora ya afya kwani serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais wake Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kwa dhati kushughulika na matatizo ya wananchi ikiwemo changamoto ya huduma za afya

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo amesema kuwa  kituo hicho kina zaidi ya  watumishi 27  wa afya  ambao wametoka katikati hospitali mbalimbali na vituo vingine vya Afya vilivyopo Jijini hapa hivyo serikali ipo katika mchakato wa kuongeza watumishi wengine katika kituo hicho na vingine ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa watumishi wa afya utakaojitokeza kutokana na uhamisho huo.

Ujenzi wa kituo cha afya Murriet ulianza Mwaka 2017 na mpaka sasa umegharimu zaidi ya  Shilingi Milioni 986, ujenzi umekamilika kwa jengo la wagonjwa wa nje na liko tayari kutumiwa na  wananchi na huduma zimeanza kutolewa ikiwemo huduma ya mama na mtoto, huduma ya wagonjwa wa nje (opd), maabara, dawa na  chanjo.

Utolewaji wa huduma za afya katika kituo cha Murriet  kutasaidia kutatua changamoto za huduma za afya kwa  wakazi wa kata ya Murriet na Jiji zima kwani utaimarisha hali ya utoaji wa huduma za afya na kupunguza msongamano katika hospitali na vituo vingine vya afya vilivyopo Jijini Arusha

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa