• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Jiji la Arusha Kutekeleza Mpango Shirikishi wa Kuthibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele.

Posted on: November 16th, 2022

Na Mwandishi Wetu
Arusha

Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wizara ya OR-TAMISEMI imeandaa mpango Shirikishi wa Kuthibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ikiwemo kichocho na minyoo tumbo kwa shule za msingi ili kulinda usalama wa mtoto na makuzi yao.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Wilaya ya Mpango huo, Mkuu wa wilaya ya Arusha Mhe. Said Mtanda amesema kuwa baadhi ya  wanafunzi wanaathirika na minyoo hivyo Serikali imeleta dawa hizo kwa lengo la kuhakikisha usalama wao.

Aidha Mhe. Mtanda amesema kuwa magonjwa ya minyoo huwa hayapewi kipaumbele katika jamii hivyo wazazi wanatakiwa kuhakikisha watoto wao wanameza vidonge hivyo ambapo zoezi hilo linatarajiwa kuanza rasmi Novemba 18 hadi 19,2022.

"Wanaohusika ni wanafunzi wote wa shule za msingi wanatakiwa kumeza vidonge kwa ajili ya kukinga magonjwa yatokanayo na minyoo hivyo wito wangu kwa walimu wa shule za msingi,Maafisa elimu kata wanatakiwa kuhakikisha wanafunzi wote wenye umri wa miaka 5 hadi 14 wanapata dozi ya vidonge,"amesema Mtanda.

Kwa upande wake Mratibu wa Mpango Shirikishi wa Kuthibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Jiji la Arusha Bi. Monica Ngonyani amesema mpango huo ni shirikishi wa kudhibiti magonjwa ambayo hayapewi kimpaumbele ikiwa magonjwa hayo ni mabusha,matende,trakoma,usubi ,kichocho na minyoo tumbo. 

Aidha amesema kuwa Halmashauri ya Jiji hilo iliingia mkataba tangu Februari 22, 2022 yenye jumla ya bajeti ya Sh. milioni 58.5 ambazo ni ruzuku kutoka kwa wafadhili RTI kwa msaada wa watu wa marekani kwa lengo la kufanikisha zoezi hilo.

"Shughuli zinazofanywa katika zoezi hilo ni pamoja na mafunzo kwenye ngazi mbalimbali,shughuli za uhamasishaji kwa njia ya gari,redio,usimamizi shirikishi ma ufuatiliaji na ukusanyaji wa taarifa,"amesema.

Amesema kuwa wanatarajia mwaka huu kufikia asilimia 100 endapo wakipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa watu mbalimbali hadi kukamilika kwake Novemba 19,2022.



Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa