• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Jiji la Arusha laweka historia Kwa kufanya Mahafali ya pamoja ya kidato cha Nne kwa wanafunzi wa shule zote za sekondari zilizopo Jijini

Posted on: October 30th, 2018

Halmashauri ya Jiji la Arusha leo Tarehe 30 Octoba 2018 imeweka historia kwa kufanya mahafali ya pamoja kwa wanafunzi wa  kidato  cha nne wa shule zote za sekondari za serikali na binafsi zilizopo Jijini Arusha.

Mahafali hayo ya kihistoria yalioandaliwa na uongozi wa Jiji la Arusha  kwa kushirikiana na wakuu wa shule zote za serikali na binafsi pamoja na wadau mbalimbali wa elimu, yamelenga zaidi kutoa fursa kwa wanafunzi ambao shule zao hazifanyi mahafali kutokana na uchumi duni ambao unawakwamisha kuchangia gharama kubwa za uendeshaji wa mahafali hayo pamoja na kutoa fursa kwa wanafaunzi wanaohitimu kuzijua fursa wanazoweza kuzitumia baada ya kumaliza masomo ya sekondari  ikiwa ni kujiendeleza kiuchumi, kijamii na kiteknolojia  hasa kwa wale watakaokosa nafasi za kuendelea na kidato cha tano.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo ambapo  aliipongeza kamati ya maandalizi ya mahafali hayo kwani ni ya kipekee kuwahi kutokea katika halmashauri  zote hapa  nchini.

Mhe. Gambo alisema kuwa wazazi wengi wamepata muamko wa kuwapeleka watoto wao shule baada ya mpango wa serikali wa Elimu Bila Malipo kuwapunguzia wazazi na walezi gharama za kusomesha watoto wao hivyo katika kukabiliana na changamoto ya uchache wa madarasa katika baadhi ya shule serikali imetenga shilingi Bilioni 3 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ambapo Bilioni 1.5 ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule za msingi na Bilioni 1.5 nyingine ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule za sekondari.

“Nichukue fursa hii pia kuwapongeza walimu, wanafunzi na wazazi au  walezi kwa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi ambapo Halmashauri ya Jiji la Arusha imeshika namba moja Kitaifa na Mkoa wa Arusha kushika namba tatu kimikoa” alisema Mhe. Gambo



(Pichani: Mmoja wa wahitimu wa elimu ya kidato cha nne (kushoto) akipokea cheti kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo katika mahafali ya pamoja kwa wanafunzi wa  kidato  cha nne wa shule zote za sekondari za serikali na binafsi zilizopo Jijini Arusha yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo Jijini Arusha leo Tarehe 30 octoba, 2018)


‘’Niwatakie kila la kheri wanafunzi wote mnaotarajia kufanya mitihani ya kumaliza Elimu ya Sekondari Tarehe 05 Novemba 2018 na  katika mkoa huu nitahakakikisha tunakwepa vitendo vya udanganyifu katika mitihani kwani vinaweza kutuletea fedheha ya kufutiwa mitihani na kuharibu sifa nzuri tuliyonayo katika Mkoa wetu” aliongeza mkuu wa mkoa huyo.

Naye  Afisa Elimu Sekondari Bw. Valintine Makuka ameipongeza Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kwa mpango kabambe wa Elimu Bila Malipo tangu aingie madarakani mwaka 2015. Kwa upande wa Jiji la Arusha hadi kufikia Juni 2018, Halmashauri ilikuwa imepokea jumla ya Shilingi 1,018,247,376.99 ikiwa ni fedha ya ada na ruzuku za uendeshaji.

Bw. Makuka ameongeza kwa kusema kuwa mahafali hayo yatasaidia kutoa mwamko wa hamasa kwa wazazi na wadau wa elimu katika kuchangia maendeleo  ya elimu kwa kushirikiana na Jiji la Arusha kama waraka wa Serikali Na. 6 wa 2015 unavyoeleza  majukumu ya jamii na wazazi. Moja Ya changamoto kuu ni chakula cha mchana.



(Pichani: Baadhi ya viongozi na wadau wa Elimu wa Jiji la Arusha waliohudhuria katika mahafali ya pamoja kwa wanafunzi wa  kidato  cha nne wa shule zote za sekondari za serikali na binafsi zilizopo Jijini Arusha yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo Jijini Arusha leo Tarehe 30 octoba, 2018)



Mahafali hayo ya aina yake yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo Jijini Arusha ulijumuisha zoezi la ugawaji wa vyeti na zawadi kwa wahitimu pamoja na walimu waliofanya vizuri katika kufundisha masomo yao pia wamiliki wa vyuo na taasisi mbalimbali walipata nafasi ya kuwaonyesha wahitimu fursa zilizopo katika shughuli za kujiendeleza katika nyanja mbalimbali za kiuchumi . 

Mahafali hayo yanatariwa kufanyika kila mwaka katika Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa