• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YA SERIKALI ZA MITAA ZASAINI HATI YA MAKUBALIANO

Posted on: February 9th, 2022

Na Mwandishi Wetu,

Arusha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Mwenyekiti wa Mawaziri wanaoshughulikia maswala ya Serikali za Mitaa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALGA) Mhe. Innocent Bashungwa amesaini makubaliano na Sekretariati ya Jumuiya hiyo ili kuweza kuboresha ushirikiano kwa lengo la kufufua uchumi kwa nchi za Jumuiya hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baaya ya kufunga mkutano wa siku tatu uliokuwa unaendelea Jijini Arusha, Mhe Bashungwa amesema makubaliano hayo yamezingatia vipaumbele pamoja na hatua za kimkakati za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Hili ni jambo muhimu sana kwa mustakabali wa uchumi wa EAC ambapo chini ya Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan tumeweza kufikia hatua hii ambayo kwa kipindi cha miaka kumi haikuwahi kufikiwa” alisema Mhe.Bashungwa.

Aidha, amesema kupitia muongozo na maelekezo ya Mhe.Rais samia Suluhu Hassan, serikali inaendela na jitihada ya kupeleka huduma kwa wannchi hasa waishio vijijinikupitia TAMISEMI, na kwamba huduma kwa wateja ndani ya ofisi ya Rais TAMISEMI imekupunguza adha ya wananchi waliokuwa wanaende Wizarani kufuata huduma hizo.

Naye Katibu Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe amesema, serikali ya Tanzania inaendelea kuhakikisha wanaboresha maendeleo ya serikali za mitaa ikiwa ni pamoja na kupeleka fedha katika kwa wananchi kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo kama vile shule, hospitali, barabara, maji na miundombinu mbalimbali.

Katika kuhakikisha kuwa makundi maalumu nayo yanapewa kipaumbele ili kuwainua kiuchumi, Pro. Shemdoe amesema kila halmashauri nchini inatoa aslimia kumi ya mapato yake ya ndani kwa makundi maalumu ya watu wenye umelavu, vijana pamoja na wanawake sanjari na kutengeneza ajira kwa kwa wakandarsi wadogowadogo pamoja na mafundi wa mtaani kwa kuwapa kazi kwenye ujenzi wa miradi ya serikali za mitaa kama vile shule na hospitali.

“Mpaka kufikia mwezi Januari mwaka huu wamejenga zaidi ya shule elfu 50 bila kuajiri mafundi kutoka nje kwakutumia mafundi wanaopatikana katika maeneo husika ,hivyo wametoa ajira kwa wazawa na kuongeza kuwa atahakikisha fedha zote zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya serikali za mitaa zinawafikia walengwa” Alisema Fro. Shemdoe.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Jumuiya ya Serikali za Mitaa Afrika Mashariki Getruda Rose Gamwera Aijuka, amesema atahakikisha kuwa jumuiya hiyo inakuwa sehemu za kukutanisha watu wa sekta mbalimbali na kuwa sehemu ya kufanya soko huria ndani ya nchi hizo pamoja na kuboresha mazingira na kuhakikisha sekta binafsi na sekta nyingine zinajumuika katika kuboresha maendeleo ya serikali za mitaa katika nchi zote.

Naye Innocent Uwimana,Rais wa RALGA na Mwenyekiti wa EALGA, amesema atahakikisha wanafanya kazi kwa kushirikiana na jumuiya ya afrika mashariki ili kuhakikisha kwamba sekta ya serikali za mitaa katika jamii ya afrika mashariki inakua na kutoa kipaumbele katika serikali za mitaa za nchi ya jumuiya ya frika mashariki.

 




Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa