• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

MADIWANI WAHIMIZWA USHIRIKIANO ZAIDI BAINA YAO.

Posted on: April 27th, 2023

Na Mwandishi Wetu 

Arusha.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Felician Mtahengerwa amewataka Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha kuachana na siasa zisizo na tija badala yake waungane kwa pamoja katika kuleta maendeleo ya wananchi wa Jiji hilo.

Mhe. Mtahengerwa ameyasema hayo katika Mkutano wa Baraza la Madiwani  wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wa robo ya tatu ya mwaka 2022/2023 ambapo amewataka pia madiwani hao kutokuwa wapingaji wa mawazo ambayo yanatolewa kwa maslahi mapana ya Halmashauri hiyo.

Aidha, Mhe. Mtahengerwa amewataka madiwani hao kusimamia miradi inayotekelezwa na Halmashauri hiyo na kutatua changamoto zilizopo kwani Baraza hilo lina mamlaka ya kusimamia vizuri mambo yote ambapo pia ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kubakikisha wanasukuma ajenda ya maendeleo katika Jiji la Arusha.

Sambamba na hayo, Mhe. Mtahengerwa amewataka viongozi hao katika mikutano yao kwa kushirikiana na makanisa na misikiti kwa umoja wao kukemea vitendo vya ulawiti na ushoga ndani ya jamii na kuwaomba wazazi kukaa na watoto wao kujua mwenendo wa maisha yao na kuwafanya marafiki ili kukitokea tofauti waweze kuwaeleza mapema.

Pamoja na mambo mengine ameeleza kuwa Wilaya ya Arusha ipo katika mchakato wa kuzikagua taasisi binafsi na shule za kulelea watoto maarufu kama Day Care kama havikiuki maadili ya jamii na nchi na endapo vitabainika kuwa vinachochea ongezeko la vitendo vya ulawiti na ushoga vitafungwa na wahusika kuchukuliwa hatua kali za kisheria mara moja.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Hargeney Chitukuro akijibu swali la papo kwa papo katika Baraza hilo amesema kuwa suala la vitambulisho vya wazee viendelee kutambuliwa na kufanyiwa kazi kwenye maeneo ya upatikanaji wa huduma katika hospitali na vituo vya afya na kuongeza kwamba kupuuziwa kwa vitambulisho hivyo katika maeneo ya utoaji wa huduma ni ukiukwaji wa sheria na kwamba jambo hilo watalifanyia kazi.

Naye Diwani wa Kata ya  Ngarenaro na Mwenyekiti wa Kamati ya huduma za Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Arusha Mhe. Isaya Doita ameahidi kufanyia kazi maelekezo ya Mkuu wa Wilaya aliyoyatoa kwa maendeleo ya Jiji ili kabla ya kumalizika kwa mwaka mwaka huu wa fedha wawe wameweka mikakati itakayoleta tija kwa wananchi wa Arusha Jiji.




Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa