• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

MAELEKEZO YA RAIS SUALA LA MACHINGA, JIJI LA ARUSHA LAANZA UTEKELEZAJI

Posted on: September 23rd, 2021

Na Mwandishi wetu 

Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kutoa maelekezo kwa wakuu wa mikoa nchini kuwapanga vema machinga, Halmashauri ya Jiji la Arusha imeanza kutekeleza maelekezo hayo ambapo, Leo September 23,2021 Baraza la madiwani la Jiji hilo limefanya kikao cha dharura chenye lengo la kupitisha bajeti ya ujenzi wa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya machinga.

Baraza hilo limepitisha bajeti ya Shilingi za Kitanzania Billioni 1 kwa kuanzia ambapo utekelezaji wa mradi huo utaanza na eneo moja baada jingine huku fedha hizo zikitolewa kwa  awamu.

Maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya machinga ni eneo la NMC Samunge, eneo lilopo jirani na stendi ya daladala Kilombero, eneo la Machame luxury, eneo la kiwanja namba 68 Kilombero,  eneo la kwa Mrombo na eneo la uwanja wa Ulezi (Florida). 

Akizungumza wakati wa Baraza hilo la Madiwani Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Mhe. Maxmillian Iranqhe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa nchini kuwapanga vema  machinga, nakueleza kuwa baada ya utekelezaji wa maelekezo hayo Jiji la Arusha litakua katika mpangilio mzuri na wenye kuvutia.

Mhe. Iranqhe amesema Arusha ni Jiji la kitalii na uchumi wake hutegemea sekta hiyo kwa kiwango kikubwa,  hivyo amesisitiza kuwa utekelezaji wa maelekezo hayo ya Mheshimiwa Rais ni hatua kubwa ambayo itaimarisha uchumi wa Jiji hilo, kwani ni hatua itakayowakaribisha watalii wengi kwa kuvutiwa na mpangilio mzuri wa Jiji , huku hatua hiyo ikidhamiriwa kuwa miongoni mwa jitihada za wazi zitakazojenga hadhi ya Jiji la Arusha inayosifika kwa majina kama 'Geneva of Africa' na California ya Tanzania.

Aidha Mhe. Iranqhe amesema mradi huo utakapokamilika machinga wataondoka barabarani, wataondoka kwenye mitaro ya maji na kuacha ujenzi holela kwenye maeneo ya 'Central Business District' (CBD).

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dk. John Pima ametoa wito kwa machinga wa Jiji la Arusha kuwa watakaopangwa kwenye maeneo yaliyotengwa ni wale ambao wana vitambulisho vya machinga, huku akielekeza utaratibu wa kujipatia vitambulisho hivyo kuwa ni kuanzia kwenye ofisi za Kata ambapo watafanyiwa tathmini ya uhalali wa kukidhi vigezo vya kuwa machinga.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Sekei Mhe. Gerald Sebastian amesema ujenzi wa maeneo hayo kwa ajili ya machinga utasaidia kurasimisha na kuwatambua machinga wa Jiji la Arusha, huku Diwani wa Kata ya Lemara   Mhe. Naboth Selasie akieleza kuwa mradi huo utakapokamilika utaboresha maisha ya wananchi.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa