• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AWAONYA MADIWANI NA VIONGOZI WENGINE WANAOKWAMISHA UKUSANYAJI WA MAPATO YA HALMASHAURI

Posted on: January 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa awaonya Madiwani na viongozi ,wanaokwamisha mapato ya Halmashauri

Na Mwandishi wetu

MKUU wa Mkoa wa Arusha  Idd Kimanta amesema hatakuwa tayari kuvumilia kuona kiongozi ama diwani  anayekwamisha jitihada za maendeleo ikiwa ni pamoja na kukwamisha ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo vya mapato na kwamba viongozi kama hao watashughuliwa kwa mujibu wa sheria .

Mkuu wa Mkoa huyo ametoa onyo hilo wakati akifungua mafunzo ya madiwani ya siku tatu yakuwajengea uwezo na kujua majukumu yao  kama wawakilishi wananchi katika Halmashauri ya Jiji la Arusha ,mafunzo yanayofanyika katika ukumbi wa mikutano ya  Halmashauri ya Jiji la Arusha

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wanajukumu la kuhakikisha mapato yanakusanywa kutoka kwenye vyanzo vya mapato  na kuonya kuwa ni marufuku kwa kiongozi kuhamasisha wananchi wasilipe mapato  na kwamba Jiji la Arusha linahitajika kukusanya mapato hadi kufikia kiwango cha Tshs billion 22 zilipangwa kukusanywa za mapato ya ndani .

 Aliwataka madiwani hao kufuata kanuni na sheria za Halmashauri pamoja na kuwa na mipaka katika utendaji na uwakilishi wa wananchi na kwamba mafunzo wanayowapatia yatawafungua na kuwafanya kujua mipaka yao .

Awali  Mkuu wa Wilaya ya Arusha Kenan Kihongosi akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kufungua mafunzo hayo aliwataka madiwani kuwa mfano bora na kuleta umoja katika Halmashauri ya Jiji la Arusha na kwamba wasiruhusu migogoro na migongano miongoni mwao .

Mh.Kihongosi alisema kuwa jukumu la madiwani ni kuhakikisha kuwa wanaletea wananchi maendeleo na kwamba maendeleo hayo yatapatikana kwa kuhimiza ukusanyaji mapato kama maagizo ya Serikali .

Alionya kauli na uchochezi wa baadhi ya viongozi wanaokwamishaji jitihada za kuhimiza wananchi kutekeleza wajibu wao wa kulipa kodi .

Kimsingi alisema kuwa agizo la Waziri wa TAMISEMI liko wazi kwamba ifikapo januari 30 mwaka 2021 kila  Halmashauri iwe imekusanya mapato kufikia nusu ya mapato iliyojiwekea kukusanya mwaka wa fedha .

Naye Meya wa Jiji la Arusha   Maxmillian  Matle Iranqhe akizungumza kwa niaba ya madiwani hao alimhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuwa watashirikiana na Mkurugenzi  wa Halmashauri  pamoja na watumishi wa Halmashauri ya Jiji kukusanya mapato ya Halmashauri .

Alisema kuwa ni wazi kuwa umoja ni silaha na kuwa watashirikiana  na watumishi wa halmashauri ya Jiji la Arusha kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba Siasa zimekwisha .

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha  Dk.John Pima akizungumzia mafunzo hayo alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Madiwani na wakuu wa Idara Halmashauri ya Jiji la Arusha kuendelea kujua majukumu yao .

Dk.Pima  alisema kuwa baada ya mafunzo haya kila mshiriki atakuwa na uwezo wakujua wajibu na mipaka yake na hatimaye kufanya kazi za kuwatumikia wananchi  kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo .

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa