• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Rais Samia na mikakati mipya kupunguza ajali barabarani

Posted on: November 23rd, 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Polisi Kitengo cha usalama barabarani kuzidi kutoa elimu hasa kwa mitandao ya kijamii, kuwekeza katika utafiti na Maafisa wa polisi kujenga ukaribu na wananchi ili kupunguza  ajali za barabarani.

Rais Samia ametoa maagizo hayo wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya wiki ya Nenda kwa usalama barabarani yaliyo fanyika kitaifa Mkoani Arusha yatakayo dumu kwa wiki moja kuanzia Novemba 23 hadi Novemba 28, 2021 Ikiwa na lengo la kupunguza ajali za barabarani, huku Kauli mbiu yake Ikiwa ni '"Jali maisha yako na ya Mwingine Barabarani''. 

"Mbali na kutumia runinga na vipindi vya redio, mnaweza kutumia mitandao ya kijamii kwasababu vijana wengi wapo huko hivyo mnaweza kuwafikia wengi zaidi...Lakini eneo la pili ni Utafiti ni vema mkafanya Utafiti ili mpate Suluhu ya kisayansi na kimfumo... askari muwe msaada kwa wananchi na si kuwa kero, muwe kimbilio la wananchi na sio mkimbiwe" -Rais Samia Suluhu Hassan.

Sanjari na hayo Rais Samia amejibu maombi kadhaa yaliyo wasilishwa mbele yake Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  SACP Wilbroad Mutafungwa,  ombi la kupata Gawio la fedha za makusanyo ya Tozo Barabarani, mitambo ya kisasasa ya ukaguzi wa magari na camera katika barabara kuu.

Rais Samia amepinga ombi la Baraza la Usalama Barabarani kupata Gawio kutoka kwenye makusanyo ya Tozo akisema kuwa kwa kufanya hivyo Jeshi la polisi litatumia nguvu nyingi katika kutoza kitendo kitakacho bugudhi watumiaji wa Barabara.

Akiendelea kujibu ombi la mitambo ya kisasa ya ukaguzi wa magari, camera katika barabara kuu, Mh. Rais Samia ametoa mapendekezo kuwa Baraza la Usalama lifungue milango kwa sekta binafsi kuwekeza katika maeneo hayo kwani ni kwa muda mrefu sekta hizo zimekua zikihitaji nafasi hizo bila mafanikio.

Katika risala fupi iliyo wasilishwa na SACP Mutafungwa imeeleza kuwa Jeshi la Usalama barabarani limefanikiwa kupunguza ajali za barabarani akitoa takwimu kwa miaka minne tangu 2018 ambapo Mwaka 2018 jumla ya ajali zote ni 3732, Mwaka 2019 ni 2704, Mwaka 2020 ni 1714 na kwa mwaka 2021 ni 1388.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Majeshi, Wakuu wa Wilaya, Wabunge, Madiwani na Wengine huku Mwenyeji wao akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongela. Mara ya mwisho Maadhimisho hayo yalifanyika Mwaka jana Mkoani Kilimanjaro.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa