• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

RC Mongella akabidhi Mikopo ya Tshs million 640.9 kwa Wanawake ,Vijana na Watu wenye Ulemavu apongeza Halmashauri ya Jiji la Arusha

Posted on: September 30th, 2021

RC Mongella akabidhi  Mikopo ya Tshs  million  640.9 kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu apongeza Halmashauri ya Jiji la Arusha. 

Na Mwandishi wetu

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella amekabidhi  Tshs milioni 640.9  ikiwa ni za mikopo kwa  Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu ikiwa ni sehemu ya mikopo ya asilimia 10 ya Fedha zinazotokana na Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Arusha. 

Mhe. Mongela akikabidhi mkopo huo katika ofisi za Kata ya Muriet, Tarafa ya Elerai  alitaka wanufaika wa mikopo hiyo kutumia mikopo kwa kuanzisha shughuli zitakazobadili maisha yao na kuwa bora zaidi. 

Mkuu huyo alitaka kurejesha mikopo hiyo kwa wakati hatimaye kuwezesha watu wengine kukopa na kujikwamua kutoka katika hali duni ya maisha. 

Mikopo hiyo  imetolewa na Halmashauri ya Jiji la Arusha  ikiwa  ya robo ya Tatu na ya Nne ikiwa imelenga  vikundi 48 vya Tarafa ya Elerai  ambavyo ni vikundi vya wanawake 34 vilivyopata mkopo  wa Tshs Milioni 364.8, vikundi vya vijana 13 vimepatiwa Tshs Milioni 273.08 na kikundi kimoja cha watu wenye Ulemavu Tshs. Milioni 3.

Mhe. Mongella  anasema  fedha za mikopo hiyo zimetolewa na Serikali  kwa lengo la kuwawezesha wananchi  kuanzisha shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja ujasiriamali hatimaye waweze kuongeza kipato na kuondokana na umaskini.

Mkuu huyo amemshukuru  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wake kuwa Mhe. Rais ametoa mikopo hiyo ikiwa  ni kuwezesha wananchi anaowaongoza kuondokana na hali duni ya maisha baada ya kupata mikopo na kuanzisha shughuli za uzalishaji  mali. 

Amepongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa kuendelea kutoa mikopo hiyo ambapo pia tayari  Halmashauri hiyo imeweza kutoa mikopo kwa vikundi Tarafa ya Suye yenye thamani ya Tshs  million 504.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dk. Onesmo Mandike amesema kwamba Halmashauri  itaendelea kutoa Mikopo hiyo kwa wakati na kutaka wananchi kujitokeza kuomba mikopo hiyo. 

Kaimu Afisa Maendeleo ya Jiji la Arusha, Bi. Tajiel Mahega, akitoa ufafanuzi wa mikopo hiyo alisema Halmashauri ya Jiji itaendelea kutoa mikopo hiyo na kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo watu na wajasirimali wanaomba mkopo lengo ikiwa ni kuwawezesha kuanzisha Biashara zitakazobadili maisha yao  kuwa bora na kuupa umaskini  kisogo.



Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa