• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI JIJINI ARUSHA WAPATIWA DAWA KINGA TIBA YA MINYOO KAMA HATUA YA KUENDELEA KUTOKOMEZA MAGOJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE KATIKA JAMII

Posted on: March 12th, 2020

Wataalamu wa afya katika Jiji la Arusha wametakiwa kuendelea kutokomeza magonjwa yasiyopewa kipaumbele kwa kuhamasisha na kuelimisha jamii juu ya umuhimu huo pamoja na kutekeleza zoezi la  kitaifa la umezaji wa dawa kinga tiba ya minyoo kwa watoto wenye umri wa miaka 5 – 14 kila mwaka.

Agizo hili limetolewa na mkuu wa Wilaya ya Arusha mapema leo Tarehe 12 Machi 2020 katika ufunguzi wa zoezi hilo linalotarajiwa kufanyika katika shule 48 za msingi zilizo za Serikali na  106 zisizo za Serikali katika Halmashauri ya Jiji la Arusha .

Ufunguzi wa zoaezi umefanyika leo Tarehe 12 Machi katika shule ya msingi Daraja mbili  na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabrieli Daqarro akiambatana na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ambaye pia ni Afisa elemu msingi Mhe. Omar Kwesiga na Diwani wa  Kata ya daraja mbili Mhe. Msofe , Mganga Mkuu wa Jiji Dkt. Herry Kagya pamoja na timu ya uwezeshaji huduma  za afya kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha (CHMT).

Akifungua zoezi hilo Mkuu wa Wilaya ya Arusha alisema kwa mwaka 2019 zoezi hilo lilifikia asilimia 92 ya utekelezaji wake na lengo kuu la mwaka huu 2020 ni kufikia asilimia 100 ambapo wanafunzi 104,986 Jijini wakiwa wavulana 52,771 na wasichana 52,215 wanatarajiwa kumeza dawa za minyoo.

Zoezi hilo litasimamiwa na walimu 3,083 na wataalamu wa afya 170 pia alisisitiza zoezi hilo likafanyike kwa ufanisi na aliwasihi waalimu waendelee kuwaelimisha watoto kuzingatia usafi wa mazingira na vyoo kwani baadaye wao ndio watakua mabalozi wazuri katika jamii.

Pia alimpongeza afisa elimu na walimu wote wa Shule ya msingi Daraja mbili kwa kuongoza kufaulisha kwa miaka miwili mfululizo kitaifa katika matokeo ya mitihani ya taifa darasa la nne na kuwaomba wataalamu wa afya wahahakikishe kuwa wanatokomeza magonjwa ambayo yalikua hayapewi kipaumbele katika Jamii .

Naye Afisa elimu msingi Mhe. Ommar Kwesiga Alishukuru  Serikali kwa utoaji huduma mbalimbali za kijamii na alipongeza juhudi za Mhe.Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa elimu bure na kuboresha miundombinu ya shule kwani imeleta mafanikio makubwa katika sekta ya elimu.

Kadhalika diwani wa kata ya Daraja mbili Mhe.Msofe alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Arusha kwa kufungua zoezi hilo la umezaji dawa kinga tiba ya minyoo kwa niaba ya Jiji zima la Arusha katika  Kata yake .

Sambamba na hilo naye Mganga Mkuu wa wa Jiji la Arusha  Dkt. Kheri alisema mwaka 2015 katika jiji la Arusha ugonjwa wa minyoo ulikua kati ya yale magonjwa 10 yanayoongoza lakini hadi hivi sasa wamesha punguza kwa kiasi kikubwa na zoezi hilo limeanza kuzoeleka katika jamii na Halmashauri ilikwisha kusaini (M.O.U) tangu tarehe 31/01/2020 yenye jumla ya bajeti ya Tshs 40,965,102.21/= ambazo ni ruzuku kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserekali kama vile (USAID) kwaajili ya ufanikishaji wa zoezi hilo ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo katika ngazi mbalimbali, kuratibu shughuli za uhamasishaji, matangazo na usimamizi wa vifaa. Pia alitoa rai kwa watanzania hususani wazazi, waruhusu watoto wao wapate dawa hizo ambazo ni salama kwa watoto wao.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa