• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

WATOA HUDUMA ZA AFYA WAASWA KUTOA ELIMU YA KUTOSHA JUU YA LISHE BORA KATIKA JAMII

Posted on: December 12th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel F. Dagarro amefungua kikao cha maandalizi ya mipango ya bajeti cha afua za lishe ambacho kimehudhuriwa na wakuu wa idara mbalimbali wa Halmashauri ya Jiji pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya afya katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya  Jiji la Arusha mapema leo Tarehe 12 Desemba 2019.

Akifungua kikao hicho Mhe.Dagarro amewasihi watoa huduma za afya kutoa elimu ya kutosha juu ya afya ya lishe kwa mama wajawazito pamoja na elimu juu ya malezi ya mtoto baada kuzaliwa na kuhakikisha mtoto ananyonyeshwa ndani ya miezi sita ya mwanzo.

Sambamba na hayo Mhe. Daqarro ameelekeza katika kliniki kuwepo na maafisa lishe  watakao toa elimu kuelekeza kuwa katika suala la upimaji wa afya watoto wapimwe vizuri ili kuvumbua matatizo mengine yanayowakumba kutokana na ukosefu wa lishe bora kwani lishe bora hujenga vyema afya ya ubongo na mwili wa mtoto.

Akiwasilisha takwimu kwa mgeni wa heshima afisa lishe wa Jiji Bi.Rose Mauya amesema  kiwango cha udumavu ni asilimia 31.8 kitaifa kwa mwaka 2018 na kwa mkoa wa Arusha udumavu umepungua kutoka asilimia 36 hadi kufikia asilimia 25.2 kwa mwaka 2018.

Pia Bi.Rose  ameainisha changamoto zinazokabili kitengo cha lishe kuwa ni baadhi ya wazazi kutozingatia umuhimu wa unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo  na wahudumu wa afya ya msingi kutokua na elimu ya kutosha ya upimaji wa maswala ya lishe.

Licha ya kuwepo kwa changamoto Bi. Rose amesema kitengo cha lishe  kimefanikiwa kuongeza  kiwango cha utoaji wa matone ya vitamin A na dawa za minyoo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kufikia asilimia 97.5, kufanya usimamizi  shirikishi katika vituo vya afya 6 na dispensary 4, kufanya upimaji wa lishe kwenye shughuli za maadhimisho  ya wiki ya unyonyeshaji na mwenge na kutembelea shule 8 za msingi na kutoa elimu kuhusu  lishe pamoja na kufanya upimaji wa hali ya lishe.

Aidha afisa mwandamizi kutoka wizara ya afya Ndg.Peter Kaswahili ameiasa jamii kuzingatia  unyonyeshaji wa mtoto ndani ya miezi 6 ya mwanzo ili kumkinga na maradhi mbalimbali pamoja na kumjenga  afya na akili .

Hata hivyo Bi. Joyce Ngegba ambaye ni afisa lishe kutoka UNICEF ameainisha sababu za utapiamlo katika jamii kuwa ni ulaji duni, maradhi, ukosefu wa chakula katika kaya, huduma duni za jamii, utunzaji duni wa makundi maalumu, ukosefu wa huduma za afya kwa jamii, uchafuzi wa mazingira, mifumo mibaya ya siasa ,vitapamoja na mila na desturi potofu.


Mwisho.

Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa