• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

Waziri Nape aipa Kongole Jiji la Arusha Zoezi la anwani za makazi

Posted on: April 12th, 2022

Na Mwandishi Wetu 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye amesema kuwa Jiji la Arusha ni miongoni mwa majiji yatakayonufaika na zoezi la anuani za makazi baada ya kuingizwa katika mfumo maalum   wa lugha za  mataifa mbalimbali utakaowezesha watalii kujua majina ya  mitaa na kupata huduma muhimu. 

Aidha amewaomba viongozi wa dini kuisaidia serikali katika utoaji wa elimu ya anuani za  makazi ili kufungua fursa za kimaendeleo za ndani na nje ya nchi ya Tanzania. 

Akizungumza na waandishi wa Habari Mkoani humo, Mhe. Nnauye alisema mkoa huo ni miongoni mwa mikoa inayofanya vema katika  zoezi la anuani za makazi. 

Hivyo alitoa rai kwa Wakala wa Barabara Mijini na Vijiji (TARURA)na Wakala wa Barabara (TANROADS)kushirikiana kwa pamoja na Wizara ili kuhakikisha zoezi hilo linakamilika. 

Alisema Mkoa wa Arusha mara baada ya zoezi hilo kukamilika utakuwa ni miongoni mwa mikoa yenye manufaa zaidi baada ya majina ya mitaa kuingizwa katika mifumo ya anuani za makazi kwaajili ya kuwezesha sekta ya utalii kukua kwani watalii watakuwa wanaangalia majina ya mitaa na kujua aina za huduma watakazozipata kupitia lugha mbalimbali za mataifa yao. 

Alisema pia ni vema katika zoezi la uwekaji majina katika mitaa mbalimbali waangalie historia za viongozi na watu mbalimbali mashuhuri wakiwemo watafiti ili wakumbukwe kwa majina yao kuandikwa katika mitaa mbalimbali kwaajili ya kutambua michango yao waliyoitoa kwa jamii mbalimbali au nchi. 

 "Wekeni majina ya watu walitumikia mambo mbalimbali katika historia ya nchi yetu ili watoto wetu wajue historia zao , kunawatu nchi hii wamefanya mema na historia zao zikumbukwe pia Arusha mtanufaika na anuani za makazi sababu ya fursa za utalii zilizopo maeneo haya"

Aliwaomba viongozi wa dini mbalimbali kutoa elimu katika nyumba za ibada ili waumini wajue umuhimu wa anunani za makazi na fursa zilizopo katika kujipatia maendeleo

"Nawapongeza Mkoa wa Arusha kwaubunifu wa karakana hii itakayosaidia uwepo wa nguzo na naomba mikoa mingine kuiga mfano huu wa kutengeneza nguzo za chuma kwaajili ya anuani za makazi"

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Dkt. Jim Yonazi alipongeza ubunifu uliofanywa na Mkoa wa Arusha kwa kuanzisha karakana ya kutengeza nguzo na kusisitiza kuwa awali kulikuwa na changamoto za mfumo lakini hivi sasa mfumo upo vizuri kwa ajili ya kuhakikisha zoezi hilo linakwenda kama lilivyopangwa. 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongella alisema kuwa kwa Mkoa wa Arusha wametumia changamoto za ukosefu wa fedha kama fursa za kutatua changamoto zilizopo katika kuhakikisha Mkoa wa Arusha na Jiji la Arusha kwa ujumla linahakikisha zoezi la anuani za makazi linakwenda vema kwani timu zimegawana kila wilaya na halmashauri za mkoa huo kwaajili ya kuhakikisha zoezi hilo linakwenda kama walivyojipangia kumaliza

"Mkoa huu unatumia fursa za anuani za makazi ili kujikwamua kiuchumi na wananchi wanatoa ushirikiano sasa tunaomba msiwe na wasiwasi Arusha hii ni ya mfano kwa anuani za makazi"

Awali Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Said Mtanda akitoa tathimini ya zoezi hilo alisema hadi sasa zoezi la uwekaji anuani za makazi linaendelea vema hadi sasa wameshakamilisha zoezi hilo katika kata 21 kati ya 25 zilizopo Jiji la Arusha. 

Alisema pia majengo yameshakamilika na wamepanga kufanya tathimini ya maeneo ambayo hawajayafikia pia hadi sasa  wameweka nguzo 2,130 kati ya  nguzo 9,554 zinazohitajika na kuongeza kuwa hadi sasa wameanzisha karakana ya kutengeneza nguzo hizo ili kukidhi mahitaji ya nguzo yanayohitajika.

Alisema walikaa chini na kutathimini changamoto kama fursa ikiwemo kufanya mazungumzo na wadau mbalimbali wa viwandani ili waweze kupata ndoo zaidi ya 200 za rangi. 

"Arusha hatuhitaji kusema tunaupungufu wa fedha bali tunatumia upungufu huo kama fursa za kujikwamua ili kuhakikisha zoezi hili linamalizika kwa wakati"

Naye Said Mabie ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi ,Mipango na Uratibu Mkoa wa Arusha ,alisema zoezi hilo kwa Mkoa wa Arusha lilianza April 12,2022 na viongozi mbalimbali walishirikishwa na  walianza kuweka alama maeneo mbalimbali na kusema kuwa mkoa huo ulipokea sh,milioni 905 .63 kwaajili ya kutekeleza zoezi hilo na walianza kutoa elimu kwa umma kuhusu zoezi la anuani za  makazi ikiwemo wataalam kupewa elimu. 

Alisema kwa Jiji la Arusha zoezi hilo limekamilika kwa asilimia 78.7 na Halmashauri ya Monduli ni asilimia 45.82 , Ngorongoro asilimia 12.51, Arusha DC asilimia 11.21,Meru Dc asilimia 4.2 , Karatu asilimia 2.59 na Longido ikiwa ni asilimia 39.04

Alimalizia kwa kuishukuru Serikali kwa kuongeza sh. milioni 10 kwaajili ya kutatua changamoto hizo ikiwemo changamoto ya mfumo wa utoaji wa anuani za  makazi na kusisitiza zoezi hilo linatarajia kukamilika Mei 31 mwaka huu lakini Mkoa wa Arusha unakamilisha zoezi hilo Aprili 30 mwaka huu. 


Matukio katika picha ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye akiongozana na Viongozi wa Mkoa wa Arusha wakati akikagua utekelezaji wa zoezi la anwani za makazi Jijini Arusha, leo Aprili 12, 2022.

 



Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa