• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Arusha City Council
Arusha City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Primary Education
      • Elimu Sekondari
      • Usafishaji na Mazingira
      • Works and Infrastucture
      • Water
      • Mipango, Uchumi na takwimu
      • Mipango miji
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Tekinolojia ya habari Mawasiliano na Mahusiano
      • Manunuzi
      • Internal Audit
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa nyuki
    • Kata
      • Baraa
      • Daraja II
      • Elerai
      • Engutoto
      • Kaloleni
      • Kati
      • Kimandolu
      • Lemara
      • Levolosi
      • Moivaro
      • Moshono
      • Murriet
      • Ngarenaro
      • Olasiti
      • Olmoti
      • Oloirien
      • Osunyai
      • Sakina
      • Sekei
      • Sinon
      • Sokon I
      • Sombetini
      • Terrat
      • Themi
      • Unga Ltd
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Usafi wa Mazingira
    • Elimu
    • Biashara
    • Maendeleo ya Jamii
    • Leseni
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Wabunge na Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maadili
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba za Vikao
      • Ratiba ya kumuona Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • STUDY ONLINE
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa umma

ZAIDI YA VIKUNDI 100 KATIKA JIJI LA ARUSHA VYAPATIWA MIKOPO, DC MTANDA APONGEZA

Posted on: November 10th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Arusha Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi hasa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kutumia fursa ya uchukuaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa lengo la kujiinua kiuchumi wao binafsi na nchi kwa ujumla.

DC Mtanda (Katikati) akiwa ameshika Hundi ya Tsh. Milioni 404.5 ambayo alikabidhi kwa vikundi wanufaika.

Mhe. Mtanda ameyasema hayo Jijini Arusha,wakati akizungumza na Vikundi Wanufaika wa Mikopo hiyo ambapo amesema kuwa zaidi ya Sh.milioni 143 zitatolewa kwa vikundi vya vijana 14 lakini wengi wao hulalamika mikopo hiyo haiwafikio kitokana na kutokupata taarifa.

"Lakini wanapopewa mikopo wahusika pengine hawaioni hivyo ni vyema tukaendelea kuwaonyesha kwamba sisi Jiji la Arusha kwamba tunatekeleza sera na maelezo ya serikali ya kutoa asilimia 10 ikiwa vijana asilimia 4,wanawake asilimia 4 na 2 kwa watu wenye ulemavu,"alisema Mtanda.

"Jumla ya vikundi 52 ambapo vikundi vingi ni vya kinamama vitapatavyo 28 baada ya kupata majibu ya vikundi vingi kuwa ni vya kinamama nilibaini kuwa ni wanawake ni wahaminifu pindi wanapopewa mikopo" aliongeza Mtanda. 

Alisema wanawake hao wanatengeneza mazingira ya kujikomboa kiuchumi ikiwemo vikundi vya watu wenye ulemavu ambapo serikali imewarahisishia sio lazima kuwepo katika vikundi bali wanatoa hata kwa mtu mmoja mmoja.

"Mtu yeyote mwenye ulemavu aliyetayari katika kujikwamua kiuchumi anapewa mikopo hata akiwa peke yake kwa hiyo sisi tunaamini kila mtu anaweza akiwezeshwa na hawa tunataka wawe mfano kwa walemavu wengine kwani wanao uwezo mkubwa na nguvu,"alisema Mkuu huyo.

Mtanda alitoa wito kwa vikundi vyote vinavyopokea mikopo kuwa waadilifu kwenye mikopo hiyo ili waweze kuaminika  na ni lazima  wawe na utamaduni wa kulipa marejesho ya mikopo hiyo ya Halmashauri na wasijiwekee matumizi mabaya.

Mkuu huyo alisema kama ni kikundi ni vyema kikawa na maendeleo ya pamoja  kwani ikumbukwe kuwa umoja ni nguvu utengano ni dhaifu.

Naye Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Jiji la Arusha,Hergeney Chitukuro alisema katika kipindi cha robo ya mwaka wametoa mikopo yenye jumla ya sh.milioni 873.6 kwa jumla ya vikundi 108.

"Lakini katika kipindi hiki tumetoa mikopo ya awamu ya pili katika vikindi 52 ambapo vimepata jumla ya sh.milioni 404.5 ikiwa mchanganuo wake ni vikundi 28 ni wanawake ambao wamepata sh.miliono 198.6,vijana vikundi 14 vimepatiwa jumla ya sh.milioni143 na watu wenye ulemavu ni vikundi 10 ambapo wamepatiwa jumla ya sh.milioni 62.9,"alisema Chitukuro.

Naye Mbunge wa Arusha mjini Mrisho Gambo ameushukuru uonhozi wa halmashauri ya jiji la Arusha kwa kuwapatia mikopo wanufaika hao kwa lengo la kujikwamua kiuchumi na kuhakikisha wanapata mikopo kama serikali ya awamu ya sita inavyoelekeza. 


Wanufaika wa Mikopo wakishiriki katika semina ya mafunzo ya kujengewa uelewa juu ya mikopo ya asilimia 10 iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Arusha School. 


Matangazo

  • NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUSAFIRI NJE YA NCHI KWA WATUMISHI WA SERIKALI January 16, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO KADA YA MTENDAJI WA MTAA NA KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU October 06, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 15, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO October 29, 2024
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • JIJI LA ARUSHA LAZINDUA MITAMBO MIPYA

    January 28, 2025
  • MKURUGENZI KAYOMBO AKABIDHIWA OFISI

    August 21, 2024
  • WANAWAKE NA WASICHANA KUJENGEWA UWEZO WA KISHIRIKI NAFASI ZA UONGOZI

    August 20, 2024
  • NENDENI MKAONGEZE UFANISI

    August 19, 2024
  • Tazama zote

Video

JIUNGE NA MFUMO WA TAUSI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MIRADI ILIYOKAMILIKA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA
  • SISI NI NANI
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira safi Maisha bora

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Tovuti ya ajira
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Location Map

Wasiliana nasi

    20 Boma Street 23101

    Sanduku la Posta: 3013

    Simu: 0272548072

    Simu ya Mkononi: 0272545768

    Barua Pepe: cd@arushacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki ©2018 Halmashauri ya Jiji la Arusha .Haki zote Zimehifadhiwa